Mshambuliaji wa zamani wa Ghana, Asamoah Gyan amefichua kuwa aliwahi kufikiria kumshambulia na kumdhuru Luis Suarez kufuatia kitendo cha Suarez kuikosesha Ghana fursa ya kutinga nusu fainali ya Kombe la Dunia mnamo 2010 huko Afrika Kusini.
“Nakumbuka mchezo kati ya Sunderland na Liverpool. Tulikuwa tukicheza nyumbani siku hiyo na wachezaji wote walikuwa wakipeana mikono,” Asamoah Gyan ameiamba Peace FM.

“Nilitaka kumpiga Suarez kwa sababu watu walisema mambo ambayo yalinikaa akilini.
“Nilikuwa mjinga wakati huo lakini nilipofikiria juu yake baadaye, niligundua kwamba nilipaswa kupotezea kwa sababu hata mimi ningefanya jambo lile (kuuzuia mpira kwa mkono) kama ningekuwa katika nafasi yake.”
Maana halisi ya ushindi mkubwa unaipata katika kasino ya mtandaoni ya Aviator kutoka meridianbettz. Andaa kapu la ushindi wa mkwanja na beti kibao za BUREEE.


