Ukicheza na Real Madrid UEFA tena katika mchezo wa mtoano, unacheza dhidi ya ile jezi yao, mashabiki wao, timu yao halafu jina lao ambalo kimsingi ni moja ya jina lililotajwa mara nyingi zaidi kwenye historia ya Uefa.
Kuna mambo matatu ya kuzingatia unapocheza na Madrid yenye hasira ya kulitaka kinguvu kombe linalowapa faraja zaidi kuliko makombe yote ulaya, La kwanza ni timu ya ushindani walio nayo viumbe hawa, na kwa miaka kadhaa iliyopita wamekua na timu ambayo wachezaji wenyewe ni mashabiki wa Real Madrid
La pili ni ukubwa wa timu yao, Madrid ni moja ya timu chache duniani ambazo hata maadui wanaokutana nao mara nyingine hua ni mashabiki zao, itakushangaza kidogo lakini hebu jiulize swali la kawaida kabisa ni nchi gani , mji gani au basi hata kijij gani kinachojihusisha na michezo na kisiwe hata na shabiki mmoja wa Real De Madrid
Hili la tatu linaogopesha zaidi. Hili linatosha kabisa kukupa mechi ngumu hata kama hawana timu imara sana au hawana nyakati bora sana uwanjani.
Hili ndilo lililowaondoa PSG siku ile! Hili ndilo lililowafikisha hatua hii na ndilo lililowafunga Chelsea jana na kuwafanya wabaki na maswali ya Jee tukiwa kwako tutatoka?. Lile jina ‘Real Madrid’ linaogopesha sana.
Katika dunia ambayo makocha wanalazimika kucheza na ‘namba tisa kivuli’ kwasababu ya uhaba wa wafungaji, yupo Karim Benzema.
Wale ni kati ya viumbe waliopo mbioni kupotea. Tembo, wale wahindi wekundu wa Amazon na Karim Benzema, wapo mbioni kupotea duniani.
3500 NI YAKO UKIJIUNGA TU MERIDIANBET!
Una nafasi ya kupata bonasi ya shilingi 3500 kwa ajili ya kuanza safari yako ya kasino ya mtandaoni ya Meridianbet.