Kocha wa Dodoma Jiji Asingizia Uchovu

BAADA ya kupokea kichapo cha mabao 3-0 mbele ya Simba, Kocha Mkuu wa kikosi cha Dodoma Jiji, Masoud Djuma amefunguka kuwa sababu ya kupoteza mchezo huo ni kutokana na uchovu wa safari.

Simba iliibuka na ushindi huo jana jumapili kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar ambapo mabao ya mchezo huo yalifungwa na Moses Phiri, Habibu Kyombo huku Abdallah Shaibu ‘Ninja’ akijifunga.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mchezo huo, Djuma alisema: “Kwanza tunamshukuru Mungu kwa mchezo kumalizika salama na hakuna mchezaji yeyote aliyepata majeraha.

“Sababu ambayo imetufanya tufungwe ni wachezaji wangu walikosa umakini kwenye eneo la mwisho na nadhani ni kutokana na ukubwa wa timu ambayo wanacheza nayo.

“Walikuwa wakifika kwenye eneo la mwisho wanakosa umakini hivyo wanashindwa kumalizia zile nafasi ambazo wanazipata.

“Kitu kingine ni kutokana na uchovu wa safari hilo pia limechangia kwani tulicheza mechi hivi karibuni na usiku huo huo tuliondoka kuja Dar hivyo wachezaji walichoka sana ndicho kilichochangia matokeo haya ya leo.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.