Guardiola Athibitisha Sane Ataondoka Man City.

Leroy sane ataondoka Manchester City hii ni baada ya Pep Guardiola kuthibitisha kuwa winga huyo kutoka Ujerumani kuikataa ofa mpya aliyopewa na timu.

City wamekuwa wakijaribu kumshawishi mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 kuongeza mkataba wake ambao utaisha 2021.

Lakini Sane ambaye amekuwa akihusishwa na kutimkia Bayern Munich miezi 12 iliyopita, amezikataa ofa mbalimbali alizopewa na klabu hiyo.

“Anataka kujiunga na timu nyingine ,”alisema Guardiola “sijui kama ataondoka msimu huu au msimu ujao kipindi mkataba wake utakapo fikia tamati.”

Sane alijiunga na Manchester City akitokea Schalke 04 kwa ada ya yuro milioni 37 (£37m) mwaka 2016.

Hajacheza tangu alipoumia katika Kombe la Ngao ya jamii (Community Shield) mwezi Agosti walipokutana na Liverpool.

Guardiola ameongea na Sane ‘mara mbili au mara tatu” kuhusiana na dili mpya akaongeza kwa kusema “tunataka kumpa mkataba mwingine sababu tuna muhitaji”.

“Ana kiwango cha kipekee. Tuna taka wachezaji ambao wanacheza kwaajili ya timu ili kufikia malengo ya Klabu.

“Ni mtu poa sana na nina mpenda, sina kitu cha kumzuia sababu anahitaji changamoto nyingine na timu nyingine.

35 Komentara

    Sane anakiwango cha kipekee ndio mana wanataka abaki ila kama hataki wamuache tu aende wakiendelea kumbembeleza wanampa kichwa

    Jibu

    Watuache tuu. Akasakate kabumbuu anakotaka. Oki awe huru.

    Jibu

    Jamani da!

    Jibu

    Sane itakua anampango wa kurudi kwao ujerumani maana wachezaji wengi wa ujerumani wanapendelea Sana kucheza nyumbani kwao

    Jibu

    Sane nenda mana maisha popote.

    Jibu

    Pengo kubwa kwa man city

    Jibu

    Safi sana ilibid tuu atumie busara kama hyo alio tumia kumuacha aendee kuliko kukaa nae alafu hampi nafasi ya kucheza

    Jibu

    Good news kwa Bayern mucheni

    Jibu

    Makala nzuri tunazipata hapa meridian

    Jibu

    Duh man cty wanampoteza mtu makini Sana.

    Jibu

    Duu! Ishakuwa pengo kubwa

    Jibu

    Yaani pengo kubwa sana kwa man city

    Jibu

    Ingawa wakuziba pengo lake kupatikana ni changamoto ila aende tu kambi popote

    Jibu

    Hilo ni pengo kubwa Sana kwa man City

    Jibu

    Bora tu aondoke Haina maana kukaa namtu ambaye akupi nafasi ya kucheza#meridianbett

    Jibu

    Sane nenda kwani maisha kokote#meridianbettz

    Jibu

    Benardo Silva amekuwa kama kiraka ndani ya Mancity lakini sasa ni wakati pia wa Mahrez kukaza ili kupata namba ya kudumu ndani ya City

    Jibu

    Leroy Anachezea maisha sana sijui utoto#Meridianbettz

    Jibu

    Ameacha gepu kwenye kikosi

    Jibu

    Mwacheni aende akaangalie fursa pengine

    Jibu

    wachezaji wengi wa ujerumani wanapendelea Sana kucheza nyumbani kwao# meridianbettz

    Jibu

    Me namshauri baki tu man city si vyema kuondoka sehemu huku bado mwenyeji wako hanakuitaji utaacha pengo kubwa kwenye clabu hiyo

    Jibu

    Daaa mia pambana

    Jibu

    Kwa nn asibaki tu

    Jibu

    Sane jembe

    Jibu

    Sa itakuaje

    Jibu

    City wanampotezah mtu makini sana

    Jibu

    Sane bado mchezani mzuri sana. Bro nenda ukatafute changamoto nyingine nakukubali sana#meridianbettz

    Jibu

    Duuh jamni kwanini

    Jibu

    Anatakiwa akatafute changamoto nyingine mahali pengine

    Jibu

    Itabidi watafute atakaeziba pengo lake

    Jibu

    Sane fundi mwenye kasi na skills za kutosha wamuache akatafute changamoto nyngine

    Jibu

    Ahsante kwa taarifa #meridianbettz

    Jibu

    Maoni:Maisha popote wacha Sane akapambane kwengine

    Jibu

    Maisha popote nenda tu

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.