Kocha wa Chelsea, Liam Rosenior, amesema kuwa kitendo cha wachezaji wake kukusanyika katikati ya uwanja kabla ya kuanza mechi hakilengi kuwachokoza wapinzani, bali kuonyesha umoja ndani ya timu.
Kauli hiyo imekuja kufuatia tukio la kushangaza lililotokea kabla ya mchezo wao dhidi ya Newcastle United ambapo mwamuzi Paul Tierney alijikuta katikati ya mkusanyiko huo wa wachezaji muda mfupi kabla ya kuanza kwa mchezo.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Baadhi ya wachambuzi wamekosoa tabia hiyo wakidai kuwa ni ukosefu wa heshima kwa wapinzani, lakini Rosenior amesisitiza kuwa lengo kuu ni kujenga mshikamano wa timu na si kuleta taharuki au presha kwa wapinzani wao.
Hata hivyo, kocha huyo hakuthibitisha kama wataendelea na utaratibu huo katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Paris Saint-Germain, akisema wataamua kabla ya mechi hiyo muhimu.
Aidha, Rosenior amethibitisha kuwa nahodha Reece James atakosekana kwa muda kutokana na jeraha la misuli ya paja, huku beki Malo Gusto naye akiwa katika hatihati ya kukosa mchezo huo, wakati Chelsea wakijaribu kupindua matokeo ya mabao 5-2 dhidi ya PSG.

