Kuna cha Kujifunza Kwenye Safari ya Soka la Alphonso Davies

Alphonso Davies – Pembeni yangu hapa nimetoka kukifunga kitabu cha Juddy Donnely. Kinaizungumzia safari ya binadamu watatu wa kwanza kwenda mwezini. Haikuwa safari nyepesi. Walitumia zaidi ya miaka 20 kuiandaa. Wakatumia miaka tisa kuishawishi serikali ya Marekani kuwapatia kibali. Baada ya mapigano mengi, hatimae waliruhusiwa na waling’oa nanga July 20 1969.

Haikutegemewa kuwa watarudi hai. Ila baada ya siku nne walitua salama pale Kaskazini mwa bahari ya Pacific. Mpaka leo majina yao wale binadamu yamesimama kwenye kuta za majengo ya NASA pale Washington DC. Neil Armstrong, Edwin Aldrin na Michael Collins. Nawaweka kando hapo kisha naufungua ukurasa wa Alphonso Davies.

Wazazi wa Alphonso Davies walikimbia Liberia kuokoa maisha yao

Wazazi wake waliikimbia Liberia baada ya vita kupamba moto mwaka 1999. Hawakuwa tayari kushika bunduki kwa ajili ya kutetea maisha yao. Hawakutaka kuendelea kupishana na maiti barabarani. Hawakutaka kuendelea kusikia sauti ya mabomu. Wakaamua kuondoka na kuishia Ghana Magharibi katika kambi ya wakimbizi. Huko ndipo walipompata Alphonso mwezi November mwaka 2000.

Alphonso Davies
Alphonso Davies

Baadae walipata mfadhili wa kuwatoa katika kambi ya wakimbizi, wakaondoka kwenda Canada Alphonso akiwa na miaka 5. Huko ndipo alipoanza maisha. Kwa kuwa wazazi wake hawakuwa na hela ya kumpeleka katika academy ya soka, alilazimika kuchezea timu ya kuwalea watoto wa mtaani kila jioni alipotoka shule. Soka lake likaanzia hapo.

Hapo ndipo alipoonekana na Vancouver Whitecaps, wakamchukua na kumpeleka katika academy yao. Baadae akapanda timu ya wakubwa. Bayern wakafanikiwa kumsajili July 2018 baada ya rais wa Barcelona kugoma kumsajili kwa kigezo kwamba hatokei taifa lenye historia ya soka. Ndiyo huyu Alphonso Davies tunayemuona leo kule kushoto kwa Bayern Munich.

Alphonso Davies
Alphonso Davies

Safari ngumu namna gani. Kutoka kupanga foleni ya chakula katika kambi ya wakimbizi hadi kuwa mchezaji bora chipukizi wa Bundesliga. Kutoka kucheza mitaani Canada hadi kupigwa buti na Lionel Messi. Safari ambayo kimawazo isingewezekana kufanikiwa kama ile ya kwenda mwezini.


Drops and Wins!

Umeijua hii? Ni promosheni kabambe ya ushindi kwenye Casino ya mtandaoni ya Meridianbet! Unaweza kushinda hadi Euro 2,000,000 leo.

Soma zaidi Ucheze

20 Komentara

    Alfonso davies dah barca wanamjua huyu mtu muulize semedo

    Jibu

    Ni kila kiti kinakua kwa sabab fulan usimdharau mtu usie mjua

    Jibu

    Story yake yakusisimua hatari usimdharau usie mjua

    Jibu

    Kweli usimzalau mtu usiyemjua story yake yakusisimua sana#Meridianbettz

    Jibu

    Duuh ana hisitolia nzuri sana ya kujifunza

    Jibu

    ana historia nzuri sana na kujifunza ni jambo la muhimu sana

    Jibu

    Inasisimua sana historia yake

    Jibu

    History yake Ni nzuri ya kujifunza
    @meridianbettz

    Jibu

    Kamala safi

    Jibu

    Makala safi

    Jibu

    Imekuwa history nzuri sana kwake

    Jibu

    historia nzuri kuna cha kujifunza

    Jibu

    Yupo vizuri napia anajituma kwenye kazi zake namuerewa kinoma

    Jibu

    Tunajifunza kitu hapa

    Jibu

    Asante kwa nakala

    Jibu

    Yuko sahihi kabisah

    Jibu

    Gud

    Jibu

    Yuko vizuri

    Jibu

    Dahhh, kweli maisha ni safari. Mungu ambariki

    Jibu

    Hakika maisha ni Safari story inasisimua.

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.