Mchezaji wa timu ya Bahrain McLaren – mwingereza Mark Cavendish, ametemwa katika orodha ya wachezaji wa timu hiyo watakaoshiriki Mashindano ya Tour de France.
Hii ni mara ya pili kwa Cavendish kutochaguliwa na timu ya Bahrain McLaren kwa miaka miwili mfululizo. Akiwa na umri wa miaka 35, Cavendish ameshinda mara 30 katika Mashindano ya Tour akizidiwa mara 4 na Eddy Merckx aliyeshinda mara 34.
Michuano ya Tour de France imepangwa kuchezwa kuanzia Agosti 29 mpaka Septemba 20 katika jiji la Nice – Ufaransa.
Mapema mwezi wa Mei, kiongozi wa timu ta Bahrain McLaren– Rod Ellingworth alisema Cavendish hakuchaguliwa kwa sababu maandalizi yake hayakuwa mazuri kutokana na mlipuko wa Corona. Cavendish ameshiriki mbio mara 24 pekee msimu huu bila ushindi wowote na mara nyingi amekuwa kama msaidizi wa madereva wenzake.
Timu ya Bahrain McLaren itaongozwa na Mikel Landa katika Mashindano ya Tour de France. Ellingworth amesema, ” mashindano ya mwaka huu yanamfaa sana Mikel, amekuwa na uwezo ulioimarika zaidi.
“Wachezaji tuliowachagua kumsaidia [Mikel] wanawakilisha wachezaji ambao wapo tayari kwa mashindano haya.”
Orodha ya wachezaji wa Bahrain McLaren kwenye Mashindano ya Tour de France.
- Mikel Landa (Hispania)
- Pello Bilbao (Hispania
- Damiano Caruso (Italia)
- Wout Poels (Uholanzi)
- Sonny Colbrelli (Italia)
- Marco Haller (Australia)
- Rafa Valls (Hispania)
- Matej Mohoric (Slovakia)
Cavendish alijiunga na Bahrain McLaren kwa makataba wa mwaka mmoja mapema mwezi Oktoba, 2019 na kuungana na kocha wake wa zamani – Ellingworth ambaye aliitumikia timu ya Sky kwa takribani miaka 10.
Drops and Wins!
Umeijua hii? Ni promosheni kabambe ya ushindi kwenye Casino ya mtandaoni ya Meridianbet! Unaweza kushinda hadi Euro 2,000,000 leo.
Hope mwaikuka
Usikate tamaa uwez jua wanakuepushia nn
Latifa juma mohamed
Asife moyo mzung anasema one day yes.
Sabrina
Duuh hatari
Dorophina
Asikate tamaa labda msimu ujao watamchagua tu
Mwajumah
Duuh atari ila asife moyo maana awezi jua wanakuepusha na nn#Meridianbettz
aisha
Kukata tamaa ni zambi
magdalena
apambane ili msimu ujao aweze kupata nafasi
Nasra
Nafasi bdo ipo akipange kwa msimu ujao
Zeiyana
Uwezo wake ushashuka sasa hivi ukiangalia kuna washiriki wengi chipukizi na wenye vipaji hadi kuimshinda yeye hingekua vizuri haendelee kua kama msaidizi kwa wenzie tu
Caroline
Mbona ana uwezo mzuri Sana lakini hawamchukui.. mhhh pengine ana matatizo mengine wanayajua wenyew
Mwanahamisi
Duuh hatari sana
Tatu
Mark Cavendish akuchaguliwavkutoka na maandalizi yake ayakuwa mazuri kutokana ugonjwa wa corona juu ya uwezo aliyokuwa nao
felister
ajipange tena msimu ujao
Lydia Emmanuel Magoti
Duu apambane msimu unakuja afanye vizuri
David Pere
Uwezo wake ushashuka sasa hivi ukiangalia kuna washiriki wengi chipukizi na wenye vipaji hadi kuimshinda yeye hingekua vizuri haendelee kua kama msaidizi kwa wenzie tu
farida ahmadi
Duh nouma Sana ila asikate tamaa
Ester jackson
Ajipange tena uwezo wake umeshuka sana
Samiah
Duuh
Furahav
Noma sana.
Latifa juma mohamed
Duuh hatari sana