Zidane: Barcelona Bado Wana Kikosi cha Ushindani.

Kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane anaamini Barcelona bado wana kikosi kinachoweza kupambana kwa kila mashindano.

Baada ya kuumaliza msimu bila kuambulia taji lolote, Ronald Koeman anakazi kubwa ya kuijenga Barca, ambao tumeona wakiuza wachezaji wao Luiz Suarez, Arturo Vidal,Ivan Rakitic, Arthur na Nelson Semedo.

Philippe Coutinho amerejea kutoka Bayern Munich ambako alitumia msimu mmoja kwa mkopo na Miralem Pjanic ametua Camp Nou akitokea Juventus wakati Messi pia ataendelea kuhudumu Barca baada ya jaribio lake la kutaka kuondoka kugonga mwamba.

Zidane, ambaye atawatembelea Real Betis siku ya Jumamosi, amesema Barca bado ipo imara katika kuleta changamoto ya kuwania taji.

Zidane: Barcelona Bado Wana Kikosi cha Ushindani.
Lionel Messi akiwa na wachezaji wenzeka wa Barcelona

“Nitaheshimu upande huo, sijui ni nini kinaendelea ndiyo maana sitaki kujihusisha. Kocha Zidane aliongea na waandishi wa habari.

“Nadhani kila klabu ina magumu yake na mambo yake, nadhani Barcelona kwa dhana ya timu na kikosi itaendelea kupambana kwa kila kitu.

“Sina shaka yoyote.

Lakini pia tumeona baadhi ya mabadiliko katika kikosi cha Real Madrid kwa kuwaachia wachezaji Jmaes Rodriguez aliyetimkia Everton, Gareth Bale akirejea katika timu yake ya zamani Tottenham kwa mkopo na Reguilon ambaye pia amejiunga na upande wa Jose Mourinho.

Mahusiano ya Bale na Zidane iliripotiwa kutokuwa mazuri kwa miezi ya hivi karibuni na mchezaji huyo kutoka Wales amesema kamwe hatojutia kuondoka Madrid.

Alipoulizwa anachochote cha kuongea kuhusu Bale, Zidane alijibu: “sitaongea chochote kuhusu Gareth Bale zaidi tunamtakia kila la kheri.


FURAHIA KASINO YA MTANDAONI

Tembelea ardhi ya maajabu ushangazwe na mengi ikiwa ni pamoja na urahisi wa kujipatia utajiri kupitia Kasino ya Meridianbet.

Cheza Sasa

29 Komentara

    Anachosema Zidane ni sahihi kwan barca wanakikosi kizuri tu wajitaidi kwenye mazoezi ili kupata matokeo mazuri msimu ujao na si kama walivyomaliza msimu kwa kutopata taji lolote

    Jibu

    Ndio kikosi bado kizur kikubwa kufanya mazoezi kwa bidii na kumsikiliza kocha mbon watapat matokeo mazuri

    Jibu

    kikubwa ni mazoezi wakijitahidi barca wataweza kufanya vizuri msimu huu

    Jibu

    Waongeze ujuzi tu barca wapo vzuri

    Jibu

    Kikosi cha Barcelona kipo vizuri

    Jibu

    Yangu macho ngoja tuone

    Jibu

    Barcelona bado kabic wanaitaji wachezaji wenye uwezo ili kufanya kikosi chao kiwe na ubora

    Jibu

    Sidhani kama kuna mtu yupo wa kukibeza kikosi cha barca pamoja na kutopata matokeo mazuri kwa baadhi ya mechi

    Jibu

    Kikubwa wajitahidi na mazoezi

    Jibu

    Wanatakiwa tuu waongeze jitihada ili mambo yakae sawa

    Jibu

    Apo wapambane na mazoezi

    Jibu

    Kikosi cha barcelona bado sana naona wao wanamtegemea sana mess koeman hana kazi kubwa kuunda kikosi na kukiweka sawa

    Jibu

    Ni kweli waongeze juhud tu

    Jibu

    Zidane anaona karibu na ni hofu tu ila sidhan kama Kikosi cha barca kile cha iniesta xavi mbele gaucho etoo kitatokea tena

    Jibu

    Ngoja tuone

    Jibu

    Kikosi cha Barcelona kipo vizuri

    Jibu

    Barcelona walivulugw na matokea ya last season

    Jibu

    Ngoja tuone sijui kama kuna maajabu yoyote

    Jibu

    Barcelona na Real Madrid zote mbili hazina vikosi shindani msimu huu naona Atletico pekee ndio imejipanga kuleta ushindani#meridianbettz

    Jibu

    Hayo ni maneno ya uoga tu sidhan kama barca ipo onfire

    Jibu

    Ngoja tuone matokeo

    Jibu

    Nadhani kila klabu ina magumu yake na mambo yake, nadhani Barcelona kwa dhana ya timu na kikosi itaendelea kupambana kwa kila kitu.

    Jibu

    Ndio kikosi bado kizur kikubwa kufanya mazoezi kwa bidii na kumsikiliza kocha mbon watapat matokeo mazuri

    Jibu

    Wafanye juhudi tuu,kikosi kiko vizuri tuu

    Jibu

    Barca wapo vizuri

    Jibu

    barcelona kweli bado wana kikosi kizuri ila wanabidi wakiimarishe zaidi ili kiwe kizuri zaidi kama zamani

    Jibu

    Barca wanakikosi kizuri kweli sijui hata wanakwama wapi

    Jibu

    Ngoj tuone msimu huuu

    Jibu

    Ligi ndio kwanza imeanza

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.