Kiungo Simba Nje Wiki Mbili

Kiungo mshambuliaji wa Simba, Peter Banda atakuwa nje ya kikosi hicho kwa wiki mbili kwa ajili ya kuuguza jeraha lake la mguu.

Ofisa Habari wa Simba, Ahmed Ally amesema kikosi chao kinaendelea na mazoezi kwa ajili ya mchezo wao dhidi ya Namungo.

“Timu iko vizuri na inaendelea na mazoezi kuelekea kwenye mchezo wetu wa kesho dhidi ya Namungo.

“Tunatambua utakuwa mchezo mgumu sana kwani mara zote ambazo tunakutana licha ya kwamba tunashinda lakini tunapata ushindani mkubwa sana kutoka kwao.

“Mchezaji mwenye majeraha mpaka sasa ni Peter Banda ambaye anasumbuliwa na majeraha ya mguu hivyo dokta amesema atakuwa nje kwa wiki mbili akiuguza jeraha.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.