KMC Yamvuta Majogoro Kutoka Mtibwa Sugar

Mchezaji nyota wa klabu ya Mtibwa Sugar Baraka Majogoro amejiunga na klabu ya KMC  kwa uhamisho huru baada ya kumaliza mkataba wake na klabu hiyo  kwa msimu wa 2022/23 ataitumikia klabu ya KMC.

Baraka Majogoro amejiunga na KMC akitokea Mtibwa Sugar baada ya mkataba wake kumalizika na klabu hiyo kuamua kutomuongezea mkataba mwingine.

Akizungumzia hilo, Baraka Majogoro alinukuliwa akisema kuwa “Nimesaini mkataba wa kukitumikia kikosi cha KMC baada ya mkataba wangu na Mtibwa kumalizika.

“Nina furaha sana kujiunga na timu hii na ninawaahidi kufanya kazi nzuri hivyo watarajie mambo mazuri kutoka kwangu.”

Mchezaji huyo wa kimataifa kutoka Tanzania mwenye miaka 26, amevichezea vilabu vya Tanzania Prison, Ndanda, Polisi Tanzania na Mtibwa Sugar.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.