Nyota Azam Aanza Kutupia Polisi Tanzania

Aliyekuwa nyota wa Azam FC, Idd Kipagwile ambaye kwa sasa anakitumikia kikosi cha Polisi Tanzania ameanza kutupia bao la kwanza msimu huu dhidi ya Dodoma Jiji.

Kipagwile amejiunga na Polisi kwenye dirisha kubwa la usajili msimu huu akitokea Azam baada ya mkataba wake kumalizika.

Kwenye mchezo wa ligi uliopigwa jana jumanne kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha Kipagwile alifunga bao pekee la Polisi kwa pelnat na mchezo kumalizika kwa sare ya bao 1-1.

Polisi Tanzania kwa sasa wanashika nafasi ya 14 kwenye msimamo wa ligi wakiwa wamekusanya pointi sita baada ya kucheza mechi 10.

Acha ujumbe