Kuelekea kwenye uchaguzi wa nafasi mbalimbali, Uongozi wa klabu ya Simba umefanya uteuzi wa wajumbe wa kamati ya uchaguzi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo jumamosi na klabu hiyo kupitia Bodi ya Wakurugenzi imewaweka wazi wajumbe hao.
“Bodi ya Wakurugenzi ya klabu ya Simba imefanya uteuzi wa kamati ya uchaguzi ya klabu hiyo.
“Kikao cha Bodi kilichoketi hivi karibuni Jijini Dar Es salaam kimeteua kamati hiyo kwa mujibu wa ibara ya 37 ya katiba ya Simba ya mwaka 2018.”

Kamati hiyo itaongozwa na Mwenyekiti wa kamati ambaye ni Boniface Lihamwike na Makamu wake Adv. Mwajuma Choggy huku wajumbe ni Richard Mwalibwa, Gerald Mongela na Juma Simba.
Je wewe hucheza Kasino Mtandaoni na umekuwa ukijiuliza ni mchezo gani rahisi na mzuri kwa ushindi? Basi Usihangaike Aviator ni rahisi zaidi kucheza na kushinda, kingine cha zaidi ni kwamba Aviator Bonanza imerudi tena Cheza zaidi ujiweke kwenye nafasi ya kushinda Samsung A23.


