Agnelli Alivyokomaa na Gigi!

Raisi wa Juventus, Andrea Agnelli anadaiwa kuwa ndiye alisisitiza kubaki kwa golikipa Gianluigi Buffon ‘Gigi” pale Allianz Stadium.

“Tunataka uendelee kuwa mmoja wetu” -Andrea Agnelli

Golikipa huyu mwenye miaka 42 kwa sasa, alirejea Italia baada ya kuutumia msimu uliopita kule PSG na amejikuta akiingia kwenye rekodi nyingine baada ya kuongeza mkataba wake wa sasa wenye thamani ya paundi milioni 1.5 kwa mwaka.

Kufikia msimu ujao, Buffon atakuwa anatimiza miaka 26 ya kucheza soka la kulipwa, ataingia kwenye rekodi nyingine ya kuwa mmoja ya mchezaji waliotumikia soka la kulipwa kwa mda mrefu zaidi.
Kwa mujibu wa Gazzetta dello Sport, Buffon aliambiwa Agnelli kuwa asalie klabuni hapo.

Buffon anasema alimwambia Agnelli kama anaona kumbakiza klabuni hapo ni chaguo sahihi basi kwake hana shaka kusalia na anafurahi kuendelea kuwepo.

Buffon anaingia kwenye orodha hii ya wachgezaji wenye umri mkubwa zaidi kutumia Serie A.

1. Italo Rossi (Pro Patria, 1951) – Miaka 52

2. Marco Ballotta (Lazio, 2008) – Miaka 44

3. Francesco Antonioli (Cesena, 2012) –Miaka 42

4. Gianluigi Buffon (Juventus, 2019) –Miaka 41

5. Alberto Fontana (Palermo, 2008) – Miaka 41

4 Komentara

    Safi

    Jibu

    Hongera buffon.

    Jibu

    Safi sana

    Jibu

    good news

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.