Kila meneja anakuwa anakumbukwa kwa mchango wa mafanikio ya klabu ambayo anakuwa anaitumikia. Wakati badhi ya meneja wakifanikiwa zaidi, David Moyes aliacha kumbu kumbu ya aina yake klabuni Manchester United.
Bosi huyu wa zamani wa Everton, hakupata mafanikio akiwa Old Traford baada ya kujaribu kuchukua mikoba ya Sir Alex Ferguson, mikoba iliyoonekana kumzidi kwa uzito. Ilikuwa ni miezi migumu 10 kwa David Moyes kudumu Man United.
Bosi huyu anaweza kuwa ni mmoja wa mabosi ambao wameacha kumbu kumbu ya kipekee klabuni hapo, kwa bahati mbaya kumbu kumbu yake si nzuri kama ilivyokuwa kwa mtangulizi wake.
Baada ya Moyes kuondoka mwaka 2014, United wamepita mikononi mwa mameneja wawili kabla ya kufika kwa Ole Gunnar Solskjaer. Moyes alisaini mkataba wa miaka sita pale United baada ya kutoka Everton, kwa bahati mbaya hata msimu haukuisha kabla ya Moyes kusepa huku Ryan Giggs akiwekwa kama meneja wa mda kumalizia msimu.
Moja ya vitu vinavyokumbukwa kwake ni pamoja na taji pekee la Ngao ya Jamii ambalo lilipatikana katika kipindi chake baada ya kuwachapa 2-0 Wigan Athletic.


Furahav
Kocha bora
Povel
Kocha mzuri sana
felister
David mayoes atakumbukwa daima
Issa
Moyes ulikua mzigo uliopewa ni timu ambayo ilikuwa na hadhi tofauti kwa levo ulizotokea huko everton