Klabu ya Arsenal imeendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa ligi kuu Uingereza baada ya kuifunga klabu ya Leeds United wakiwa nyumbani kwao.
Washika mitutu hao wa London ambao wamekua kwenye kiwango bora sana msimu huu wamefanikiwa kupata ushindi wao wa tisa katika michezo kumi waliyocheza msimu huu kwenye ligi kuu ya Uingereza huku wakipoteza mchezo mmoja pekee.
Klabu ya Arsenal ambayo imefikisha alama 27 leo na kuendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi kuu ya Uingereza huku wakifuatiwa na klabu ya Manchester City wenye 23 ambapo wakiwa hawajacheza mchezo wao dhidi ya Liverpool.
Bao la bukayo Saka lilitosha kuwapa Arsenal ushindi na alama tatu safi kabisa pale katika dimba la Elland Road huku klabu ya Leeds United nao wakitoa ushindani mkubwa katika mchezo huo dhidi ya vinara hao wa ligi kuu yas Uingereza.
Washika mitutu hao wa London msimu huu wanaonekana kama timu ambayo imejijenga na inaweza kutoa changamoto kubwa kwenye mbio za ubingwa.

