Bado Sijui Ninachokitaka -Zlatan Ibrahimovic

Nyota wa AC Milan, Zlatan Ibrahimovic ameweka wazi kuwa hana uhakika juiu ya Hatma yake Milan. Staa huyu pia amesisitiza kuwa bado hajafahamu ni nini anachokihitaji kwa sasa.

Zlatan amesema mambo yamekuwa yakibadilika kwa kasi kila siku kiasi kwama sio rahisi kufahamu nini kitatokea. Alirejea kutoka MLS mwezi Januari alipokuwa LA Galaxy na kutoa mchango mkubwa klabuni hao kwenye michuano ya Coppa Italia na Serie A.

Staa huyu amefunga magoli 4 katika mechi 10 za Serie A na Coppa Italia, mkataba wake unaisha mwezi Juni na inaripotiwa kuwa staa huyu mwenye miaka 38 hataweza kuongeza mkataba.

Kwa upande wake anasema bado hajajua nini anataka

“Tutaona, Sijajua nini nataka bado, Kitu kipya kinaonekana kutokea kila siku. Italia ni nyumbani kwangu kwa pili na ilikuwa safi kucheza tena San Siro.”

-Zlatan Ibrahimovic

Staa huyu anasema kwa sasa hatakiwi kuendelea kufikiria kuhusu yeye tuu, anahitaji kufurahia maisha yake na wapendwa wake kwa kuwa ana familia ya kuiangalia. Maneno ya Ibra yanaashiria kama hatarajii kusalia Milan baada ya kumaliza mkataba wake.

2 Komentara

    Hata hvyo umri umeenda tulia tu

    Jibu

    Zlatan jembe tu

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.