Beki wa klabu ya Chelsea Trevoh Chalobah amefanikiwa kuongeza mkataba na klabu hiyo mpaka mwaka 2028. Beki huyo atendelea kusalia darajani mpaka mwaka 2028 kama mkataba wake unavyoeleza.
Beki huyo ambaye amepandishwa kutoka kwenye shule ya kukuza kipaji ya klabu hiyo maarufu kama Cobham, Amekua kwenye ubora mkubwa toka amepandishwa kwenye kikosi hicho chini ya mwalimu Thomas Tuchel.
Chalobah ameeleza furaha yake wakati anaongeza mkataba na klabu hiyo “Ninajiskia furaha sana kuongeza mkataba huu, Na nitatoa kila kitu kwajili ya klabu hii” Beki huyo pia ana nafasi ya kuwepo klabuni hapo mpaka 2029 kwani mkataba wake una nafasi ya kuongeza mpaka mwaka 2029 kabla haujamalizika ambao anautumikia.
Beki huyo ambaye alipata nafasi ya kucheza timu ya wakubwa chini ya kocha aliyepita klabuni hapo Thomas Tuchel amekua akiborsha uwezo wake kadri siku zinavyokwenda na ndio sababu kubwa ya klabu ya Chelsea kumuongezea kandarasi ya kusalia klabuni hapo.
Chalobah anaendelea kuendeleza idadi ya wahitimu wa Cobham kwenye timu ya kwanza ya Chelsea akiungana na kina Mason Mount, Reece James, pamoja Conor Gallagher.

Je wewe hucheza Kasino Mtandaoni na umekuwa ukijiuliza ni mchezo gani rahisi na mzuri kwa ushindi? Basi Usihangaike Aviator ni rahisi zaidi kucheza na kushinda, kingine cha zaidi ni kwamba Aviator Bonanza imerudi tena Cheza zaidi ujiweke kwenye nafasi ya kushinda Samsung A23.

