Golikipa mkongwe wa klabu ya Celtic na timu ya taifa ya Scotland, Craig Gordon amewaaga rasmi mashabiki, wachezaji na viongozi wa klabu hiyo kwa kuweka wazi kuwa msimu ujao wa ligi utakapoanza atakuwa na timu nyingine.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 37, mpaka sasa ameshacheza jumla ya michezo 242 akiwa na kikosi cha Celtic ndani ya miaka 6 aliyoitumikia klabu hiyo.

Craig Gordon, aliyewahi kuichezea timu ya Sunderland, hivi karibuni alipewa mkataba mpya na klabu yake ya Celtic lakini akagoma kuusaini. Mkataba huo unasemekana kuwa ulikua umeounguzwa vipengele vingi sana kwani klabu ilizingatia uwezo wa golikipa huyo hivi sasa pamoja na umri ikumbukwe kuwa Gordon hivi sasa amepoteza namba katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo kwa golikipa mwingine Fraser Forster.
Pamoja na kuwa na maongezi na vilabu vingine, Gordon pia anaifikiria ofa ya kurejea katika timu yake ya zamani, Hearts!
Golikipa huyo mahiri atakumbukwa sana na wachezaji wenzake, benchi la ufundi pamoja na mashabiki wa Celtic kutokana na mafanikia aliyoyapata akiwa na timu hiyo. Gordon, akiwa na Celtic aliweza kushinda ubingwa wa ligi kuu Scotland mara 6, vikombe 5 vya ligi na Scottish Cup mara 3!

“Nimekuwa na miaka sita yenye mafanikio sana katika career yangu nikiwa hapa. Ningependa kuchukua fursa hii kumshukuru kila mtu aliyewezesha hili kwa namna moja au nyingine.” Alichapisha Gordon katika ukurasa wake rasmi wa mtandao wa Instagram.


Mariam mtandama
Hongera yake
Ester jackson
Kila la heri katika safari yako ya mechi nyingine ukapate pia mafanikio ya vikombe
Dorophina
Atafute sehemu nyingine ambayo atakuwa anacheza coz umri haujaenda sana
Magdalena
Duh kila la kheri uko aendapo
Genia Sikaluzwe
Ahsant meridianbet kwa taarifa
Fatina mfingi
Safar njema
Caroline
All the best
felister
Gordon atakumbukwa
isha
Kila la kheri uende salama
Lydia Emmanuel Magoti
Safari njema napongezi kwakwe
Theckla
Kila la kheri
lombo
Gud news
Hamidu
Asante kwa update za michezo#meridianbettz
Revina
Craig Gordon amewaaga kishujaa kwa sababu anajua anachokifanya ,ni jambo la heri kwake.
Flomena
Kila lakheri aendako
Zeiyana
Habari mbaya kwa mashabiki wa Celtic na uwongozi kwa jumla bado walikua wanatamani sana uwepo wako ila ndio hivyo tena hawezi kupinga maamuzi yako safari njema uko uwendako Craig gordon
Khadija
Kila la kheli katika safari yake aendayo#meridianbettz
Johnmary joel
Inapendeza na kufurahisha kuona unaondoka Mahali bado unapendwa kwa uwezo wako wa michezo#meridianbett
Issa
Gordon aliitendea haki nafasi yake vizuri akiwa na celtic kwa kipindi chote alipokuwa hapo na kuifanya ipate mataji mengi sana.
Christopher
Hongera Yake, sasa atafute klabu nyingine
Shafii
Ni jambo La kheri akapambane clubu zingine kwani maisha ni popote
Njiku
Nipo poa acha mchizi Gordon astafu maana age ishakata miaka 37 sio poa kakinukisha sana
Ernest
Kila la kheri Gordon
warda
Kafanya vizuri kuaga#Meridianbettz
Gabriel
Craig Gordon kafanya vzur sana akiwa Celtic 👍 kila la her
# 👏👏👏
Hope mwaikuka
Kila heri uendako na hongera kwa kaz
Sadick
Wakati fulani nilifikiri angesajiriwa na timu kubwa zaidi. Craig Gordon amestaafu kwa heshima#meridianbettz
Rehema
Kila la kheri gordon
Furahav
Hongera
Omary lukumbi
Kila la kher na kwenda kuanza.maisha mapya msimu ujao
Salma
Kila la kheri
Saupha mohamed
Safari njema
David Pere
Mafanikio alihowapatia yanatosha Sana kujivunia
Aziza mushi
Ki la la kheri
Tatu
Kila la kheri huko aendako
Povel
Kila la kheri nyanda Bora wa muda wote celtic
Neema juma
Kila la kheri huko aendako
Samiah
Kila la kheri aendako
Devotha
All the best
Amiri Kayera
Akapunzik regend kasaidia san
Angelina
Kila kheri kwake
Sabrina
Maoni:Ustaafu kwa amani Craig Gordon