Eddie Nketiah Hauzwi - Mikel Arteta

Mkufunzi wa Arsenal Mikel Arteta amekanusha uwezekano wa Eddie Nketiah kuihama klabu hiyo katika dirisha la usajili la mwezi Januari.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 yupo katika miezi sita ya mwisho ya kandarasi yake kwenye Uwanja wa Emirates na anaaminika kuwa kwenye mazungumzo ya kuhamia Crystal Palace.

Kuelekea mechi ya kwanza ya nusu fainali ya Kombe la EFL dhidi ya Liverpool, Arteta alisisitiza kwamba Muingereza huyo hataelekea kwingine wakati wa majira ya baridi.

Eddie Nketiah
Eddie Nketiah

“Hali ni kwamba Eddie ni mchezaji wetu na Eddie atasalia hapa kwetu. Ni mchezaji wetu na yuko chini ya mkataba, kwa hivyo atakuwa nasi,” Arteta

Nketiah ameona nyavu mara matano kwenye mechi tatu za Kombe la EFL msimu wa 2021-22, lakini amecheza dakika 38 pekee kwenye Ligi Kuu msimu huu.

Kinda huyu wa Uingereza anajivunia jumla ya mabao 18 na asisti moja katika mechi 72 akiwa na Arsenal akitokea akademi yao ya Hale End.


JIACHIE NA ALMIGHTY AZTEC

Ni muda wako kujiachia na mchezo maridhawa wa Almighty Aztec katika kasino bomba za meridianbettz. Nafasi ya kutengeneza mkwanja iko mikononi mwako kazi ni kwako.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.