Baadhi ya wachezaji wanataabika kwenye vikosi vyao kwa sababu mbalimbali msimu huu. EPL inawakosa baadhi ya wachezaji ambao waliwahi kuwa na sifa za kuvutia kwenye ligi hiyo.
Kuelekea usajili wa dirisha dogo mapema Januari Mosi, 2021. Baadhi ya wachezaji pengine ndio muda wao wa kutoka kwenye vifungo walivyopo kwa sasa kwenye klabu zao.
Tuwaangalie baadhi ya wachezaji wanaotabika msimu huu kwenye EPL.
Marcos Rojo – Manchester United.

Rojo alikuwa mchezaji muhimu kwenye safu ya ulinzi ya Timu ya Man United kabla ya maisha kumuendea kombo na alitolewa kwa mkopo msimu uliopita. Japokuwa maisha yake ndani ya klabu ya Estudientes hayakuenda sawa kutokana na mlipo wa COVID19, alirejea United na hayupo kwenye kikosi cha timu hiyo kinachocheza EPL msimu huu.
Newcastle na Sheffield United ni miongoni mwa vilabu vinavyotajwa kuhitaji saini ya Rojo kwa mkataba wa mkopo mwezi Januari. Endapo taarifa hizi zitakuwa na uhalisia, pengine hiyo itakuwa ni njia sahihi kwa mchezaji huyu ambaye bado anamkataba wa miezi 6 na United.

Muingereza huyu ni miongoni mwa wachezaji ambao hawana namba kwenye kikosi cha United. Safu ya ulinzi chini ya Ole Gunnar Solksjaer inatawaliwa na Harry Maguire na Victor Lindelof. Uwezo wa walinzi hawa haufanani kabisa na kiwango cha Jones.
Licha ya kwamba Jones anakumbwa na majeruhi ya mara kwa mara, bado hayupo kwenye kikosi cha United msimu huu na inasemekana yupo kwenye orodha ya wachezaji wanaouzwa na timu hiyo.
West Brom na Derby County ni timu zinazohusishwa na usajili wa Jones mapema mwezi Januari.

Bila shaka uwezo wa Origi akiwa kwenye nafasi ya kufunga goli sio wa kutilia shaka. Kwa mashabiki wa Liverpool hupenda kumuita ‘Super Sub’, hii inatokana na uwezo wake wa kuzitumia nafasi anazozipata akitokea benchi.
Safu ya ushambuliaji ya Liverpool ipo na wachezaji wenye uwezo mkubwa zaidi ya Origi. Mo Salah, Mane, Firmino na usajili wa Diogo Jota na Takumi Minamino ni dhahiri Jurgen Klopp hamuhitaji Origi kwenye kikosi chake.
Kocha wa Wolves – Nuno Espirito Santo anatajwa kama mwokozi wa Origi kutokana na kuwa na uhaba wa washambuliaji kwenye kikosi chake. Raul Jimenez bado anaendelea na matibabu na atakuwa nje ya uwanja kwa muda, hii inawapa fursa Wolves kumtizama Origi kama mbadala sahihi wa kuziba pengo hilo.

Japokuwa ndiye mchezaji anayepokea mshahara mrefu zaidi kwenye kikosi cha Arteta, Mesut Ozil hayupo kwenye mipango ya kocha huyo kuanzia kwenye michezo ya EPL msimu huu mpaka kwenye mashindano ya Europa.
Pengine dirisha la usajili la Januari ndio lilikuwa fursa ya Ozil kuondoka Emirate lakini mchezaji huyu amegoma kuondoka kwa mujibu wa wakala wake – Ozil ataendelea kubaki Arsenal mpaka mwishoni mwa mkataba wake.
Ni nini kitatokea kunako EPL kwenye dirisha la usajili mwezi Januari? Nani atabaki na nani ataoneshwa mlango wa kutokea? Weka maoni yako kwenye kisanduku cha maoni.
Hakika EPL kunajambo litatokea msimu huu!!!
VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini???



Ernest
Januari hapatoshi kwenye usajili bado macho kwa Mancity juu ya Messi
Caroline
Safi saaaana
Hopemwaikuka
This news is very complicated
Dorophina
Dirisha dogo la usajili patakuwa hapashikiki
Issa
Msimu wa kuvunja rekod
Mwanahamisi
Safi sana
Adelta
Hapo mambo yanazidi kunoga
Shakila mrope
Msimu wa kuvuna pesa huu
aisha
Imekaa powa sana
Saupha mohamed
Safi sana
Asia Abdy
Mambo n moto
Lydia Emmanuel Magoti
Hiko poa sana
David Pere
Januari hapatoshi kwenye usajili bado macho kwa Mancity juu ya Messi
Fatina mfingi
Safii
farida ahmad
Imekaa poa
Tatu
Mambo hayo
warda
Wote wanauzika tu