Ile michuano ya wanawake imeahirishwa mpaka mwaka 2021, naam, ni ile ya women’s Under-17 World Cup ambayo ilipangwa kufanyikia India mwezi Novemba mwaka huu, kwa sasa imesogezwa mbele kwa miezi mitatu, FIFA walisema hayo siku ya Jumanne.
Hii inakuwa pigo lingine kwa wapenda michezo baada ya michezo mingi duniani kusimamishwa kwa muda.
Michuano, iliyopangwa kufanyika katika majiji matano, kwa sasa itaanza mnamo mwezi Februari ifikapo tarehe 17, bodi ya michezo inayoongoza mashindano hayo iliweka wazi suala hilo.
India inatarajiwa kuongeza umaarufu wake kimataifa kwa kuwa wenyeji wa michuano hiyo na imekuwa hivyo mara baada ya kusimamia michuano ya Under-17 World Cup mwaka 2017 kwa upande wa wanaume.
“Waandaaji wote katika majiji yaliyopangwa wameweka juhudi zao na kuelekeza nguvu zao zote mpaka sasa katika kuhakikisha mambo yanakuwa sawa kabisa, nasi tunayo furaha kwani tarehe mpya zilizotajwa zitawapa nafasi wao kujiandaa vyema zaidi kwa muda walioupoteza mwanzoni na kusonga mbele zaidi.” Kamati ya ndani ya uandaaji wa mashindano hayo ilisema hayo mara baada ya tangazo hilo la FIFA.
Pia, FIFA wameweka wazi juu ya tarehe mpya za michuano ya mwaka huu ya U-20 Women’s World Cup inayofanyika kule Costa Rica na Panama. Kwa sasa itachezwa ifikapo mwezi Januari tarehe 20 mpaka mwezi Februari tarehe 6, 2021.
Na kwa upande mwingine tena michuano ya mwaka 2020 FIFA Futsal World Cup iliyopangwa kufanyikia huko Lithuania imesogezwa mpaka mwezi Septemba tarehe 12 mwakani.
Kwa wakati huu, mkutano wa 70 wa FIFA ambao ulitakiwa kufanyika nchini Addis Ababa utafanyika kwa njia ya mtandao ifikapo mwezi Septemba tarehe 18 mwaka huu.
Michezo mingi duniani imesimama kwa muda kutokana na uwepo wa mlipuko wa ugonjwa wa Corona na kuathiri michezo mingi duniani ingawa mingine inachezwa bila ya uwepo wa mashabiki.
Kuna ligi ya South Korea iitwayo K-League imerudi Ijumaa iliyopita na ligi ya Ujerumani, Bundesliga inarejea hewani leo hii bila ya uwepo wa mashabiki viwanjani.


Theckla
Ni wazo zuri kusogeza mbele kutokana na hali halisi iliyopo duniani
Tatu
Ni vizuri maana hali ya ugonjww wa corona bado aujakaa sawa
Adelta
Asante meridianbet mko vzur kwa habar za kijanja
lombo
dah hii lig inakuwa na magoli sana meridianbet pesa nje nje
mwakalosi
Mwaka 2021 kutakuwa na mashindano mengi sana
Zeiyana iddi
Ni vizuri vigezo na masharti vizingatiwe..!juu ya ugonjwa huu
Ester mmakasa
Sio mbaya kama iko kwenye utaratibu maalum na viongozi wanalifwatilia hilo ,hali itakapokuwa shwari mambo yataendelea.
Dorophina
Dhaa Corona imeharibu michezo mingi lkn Ni vizuri kuepuka maambukizi ya corona
Hamidu
Ya ni maamuzi mazuri kusogeza mbele mashindano u17 ya wanawake.! safi kwa habari moto moto za michezo# meridianbettz.
frank patrick
Pole sana kwao kwa kukosa.mashindano yao ya msingi kabisa ya ukuaji wao wa kisoka kimataifa
Povel
Asante meridian kwa taarifa za Kimichezo za Moto moto
Aziza mushi
Mm nilikuwa sijui asanten meridian kwa habari Kama hizi
winfrida
tukaze moyo mambo yakikaa sawa mchuano utaendelea
Ernest
Corona ni janga la Dunia nzima, hakika tunahitaji kupambana nalo kwa kila mbinu.
Neema hassan
Afya muhimu,mashabiki tuendelee kusubr Hadi Hali itakapokaa sawa..
Carolyne
Corona imevuruga mambo.
Hope mwaikuka
Hali bado aiko shwar so ni vzur tu
Asia Abdy
Mungu atusaidie janga lipite
felister
tuombee mungu hili janga liishe na mambo mengine yaendelee
Gabriel
Daaah! Sio mbaya japo nayo n ligi ambayo inaburudisha
Antony Luseno
Wamefanya maamuzi mema maana hali bado haijatulia
aisha
wamefanya maamuzi dhabiti
Genia Sikaluzwe
Duuuuh Corona siyo poa