Ansu Fati ni mzaliwa wa Guinea – Bissau anaye kipiga kwenye timu ya Barcelona ni mshambuliaji wa pembeni anaye tumia vyema mguu wake wa kushoto, amekuzwa na kulelewa katika kituo cha kufundishia soka cha la masia katika klabu ya Barcelona.

Kinda huyo aliye na umri wa miaka 17 aliwahi kutajwa kuhusishwa na uhamisho wa kwenda timu ya Juventus lakini taarifa hizo zilikanushwa kipindi cha nyuma.
Fati ambaye alikwezwa ngazi kutoka akademia ya Barcelona kuchezea kikosi cha kwanza msimu huu, aliweka historia Septemba 2019 kwa kuwa mchezaji wa umri mdogo zaidi Camp Nou kuwahi kufunga bao ndani ya jezi za wapambe hao wa Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga)
Kuchezeshwa kwake katika msururu wa mechi za baadaye katika La Liga na Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) kulichochewa pia na jeraha lililokuwa likiuguzwa na nahodha Lionel Messi ambaye alikuwa mwingi wa sifa kwa chipukizi huyo hasa baada ya ushirikiano mkubwa kati yake na sajili mpya Frenkie De Jong kuwatatiza sana mabeki wa vikosi pinzani.

Kulingana na Valverde, Fati ana uwezo wa kumpiku Cristiano Ronaldo wa Juventus na timu ya taifa ya Ureno na kufikia kiwango cha Messi hivi karibuni. Kufikia sasa mwishoni mwa mwaka 2018 Fati ambaye kwa sasa kiwango chake kinalinganishwa na cha chipukizi Kylian Mbappe wa Paris Saint-Germain (PSG) na timu ya taifa ya Ufaransa, bado hakuwa amechezea taifa lake la Guinea-Bissau.


Ester jackson
Habari nzuri kuna wanamichezo wenyekipaji zaidi ya cr7 na mess nimeipenda hii
Povel
Dogo fundiii sana
Hope mwaikuka
Jamaa ni hatarii sana
Gabriel
Ansu Fati n kiungo mzur yaan wakimpata timu kama Arsenal itasaidia sana maana aina ya mpira wake unaendana na club hiyo
Theonestina
Namkubali sana uyu kiungo
Elika
Dogo yuko vizur sana
David Pere
Dogo anatisha Sana na Ndio atakuwa mrisi wa Messi pale Barcelona
Evaluziga
Uyu dogo fundi sana
Tahiya
Hatimaye mrithi wa Messi hapatikana
Rehema
Namkubali sn
Mwanaidi
Huyo jamaa yupo vizuri
felister
ahsanteni kwa kunijuza hili mm nilikua sijui Kama kuna wachezaji wengine wana vibaji zaidi ya Ronaldo na messi
Genia Sikaluzwe
Huyo jamaa ni fundii wa mpira
Caroline
Ansu fati ni habari nyingine
Hamidu
Dogo anajua Sana mpaka anakera#meridianbettz
Dorophina
Yupo vizuri sn jamaa
Samiah
Jamaa yupo vizuri sn
Zeiyana
Vizuri sana kocha kumjenga mchemzaji mbadala ya wengine soka litazidi kua tamu ukimuona ansu fati umemuona messi hau lonaldo safi sana
Amani
Ansu Fati n kiungo mzur yaan wakimpata timu kama man United itakuwa poa sana# meridianbettz
Furahav
Apambane sasa.
Theckla
Anakuja kasi sana
isha
Namuona kama mwendokasi
Ernest
Ansu ni mchezaji chipukizi ambae atakuja kusumbua ulimwengu wa soka hapo baadae
Shafii
Ansu aendelee kupambana asibweteke kwa kiwango anacho kionesha apambane afike mbali
Lydia Emmanuel Magoti
Ansu Fati nikiungo mzuri Sana anajua dogo huyo apambane hafike mbalili
Sadick
Inafurahisha kuona mchezaji anayekuuzwa na Academy ya Club na kupata nafasi ya kupanda ngazi ya juu. Kila la kheri Ansu Fati#meridianbet
Mwajuma
Ajitahidi afate nyayo za cr 7
Salma
Mrithi wa messi dogo fundi
lombo
dogo yuko vzur anajitahid kwa upande wake
Emmy cleopa
Yuko vizur sana
Magdalena
Ni mchezaji mahili Sana ila awezi kumfikia Messi
warda
Tutamleta Msimbazi#Meridianbettz
Agness
Yuko vizuri namkubali
Issa
Ansu fat jembe