Klabu ya Bayern Munich kutoka nchini Ujerumani inaelezwa wamemalizana na kiungo wa kimataifa wa Ureno Joao Palhinha anayekipiga kwenye klabu ya Fulham na wako mbioni kumsajili kiungo huyo.
Kiungo Joao Palhinha yuko tayari kujiunga na wababe hao wa soka la Ujerumani na ameshakubaliana na klabu hiyo suala mshahara na klabu hiyo, Hivo kinasubiriwa ni Bayern Munich kulipa ada ya uhamisho kwa klabu ya Fulham.Ikumbukwe dirisha kubwa lililopita mabingwa hao wa zamani wa Ujerumani walikaribia kumsajili mchezaji Joao Palhinha lakini dili liliharibika dakika za mwisho kabisa, Jmabo ambalo lilimfanya kiungo huyo kutopendezwa na hali hiyo kabisa na kuilaumu klabu yake ya Fulham.
Kipengele cha mkataba aliosaini Palhinha ndani ya Fulham akitokea Sporting Cp ya ureno kinaeleza klabu yeyote itakayomhitaji inapswa kulipa kiasi cha €45 milioni, Hivo kazi inabaki kwa klabu ya Bayern Munichkulipa kiasi hicho ili kumpata mchezaji huyo ambaye anaonesha ya kuhitaji nia ya kucheza klabu hiyo.Kama ni Ng’ombe Bayern wamebakiza mkia tu kwani wanatakiwa kulipa kiasi cha pesa tu ambacho kitamruhusu kiungo huyo kuondoka ndani ya Fulham na kuweza kujiunga nao, Klabu hiyo imeonesha kumuhitaji kwa kiwnago kikubwa kiungo huyo kwani licha ya kumkosa dirisha kubwa lililopita lakini wamerudi tena kuhitaji saini yake.
This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.
Strictly Necessary Cookies
Strictly Necessary Cookie should be enabled at all times so that we can save your preferences for cookie settings.
If you disable this cookie, we will not be able to save your preferences. This means that every time you visit this website you will need to enable or disable cookies again.