Bayern Munich Washusha Beki wa Kijapan

Klabu ya Bayern Munich imefanikiwa kukamilisha usajili wa beki mpya klabuni hapo raia wa kimataifa wa Japan Hiroki Ito kwa dau la €30 milioni kutoka klabu ya VFB Stuttgart.

Bayern Munich chini ya Vicent Kompany ina kazi moja tu kusafisha wachezaji ambao hawafai klabuni hapo na kusajili wachezaji wenye ubora mkubwa ili kurejesha utawala wa klabu hiyo katika ligi kuu ya Ujerumani na hata barani ulaya ambapo wamekua wakipitia wakati mgumu kwa muda sasa.bayern munichBeki Hiroki Ito mwenye umri wa miaka (25) amekua na msimu mzuri kwenye ligi kuu ya Ujerumani akiwa moja ya wachezaji muhimu kwenye kikosi cha VFB Stuttgart ambacho kimefanikiwa kumaliza nafasi ya pili kwenye ligi kuu ya Ujerumani juu ya klabu ya Bayern Munich ambao walimaliza nafasi ya tatu.

Beki huyo amesaini mkataba wa miaka minne ambapo utamuweka klabuni hapo mpaka mwaka 2028 huku kukiwa na kipengele cha kuongeza mwaka mmoja mpaka mwaka 2029, Huu unakua usajili wa kwanza wa kocha Vicent Kompany ndani ya klabu ya Bayern Munich.bayern munichBaada ya beki huyo wa kimataifa wa Japan kusajiliwa klabuni hapo hii inaonesha dhahiri kua tetesi zinazomhusu beki wa kimataifa wa Uholanzi De Ligt kutimka klabuni hapo zinaweza kutimia, Kwani beki aliyesajiliwa ni beki wa kati na De Ligt ni beki wa kati na amekua hapati nafasi ya mara kwa mara klabuni hapo.

Acha ujumbe