Manuel Neuer Arejea Rasmi

Nahodha wa klabu ya Bayern Mnunich Manuel Neuer ambaye alikua akisumbuliwa na majeraha ya muda mrefu imearifiwa atarejea kuitumikia timu hiyo rasmi katika mchezo wa ligi kuu ya Ujerumani hapo kesho.

Manuel Neuer atarejea kesho katika mchezo wa ligi kuu ya Ujerumani dhidi ya klabu ya Darmstadt ambapo inaelezwa ataanza katika mchezo huo na taarifa ya kurejea kwake imetolewa na kocha klabu hiyo Thomas Tuchel.manuel neuerGolikipa huyo ambaye amekosekana kwa takribani mwaka mmoja sasa langoni mwa klabu ya Bayern Munich na timu ya taifa ya Ujerumani kutokana na majeraha aliyoyapata katika ajali aliyoipata mwaka jana mwishoni.

Klabu ya Bayern Munich ilipitia kipindi kigumu wakati wa majeraha ya nahodha wake huyo kutokana na mbadala wake kua changamoto,Kwani wote waliocheza nafasi yake wakati akiwa hayupo hawakufanikiwa kuvaa viatu vyake ipasavyo.manuel neuerGolikipa Yann Sommer aliyesajiliwa katika majira ya baridi mwezi Januari mwaka huu kwajili ya kuvaa viatu vya gwiji huyo tayari ameshatimkia nchini Italia katika klabu ya Inter Milan, Hivo Manuel Neuer anarejea klabuni hapo moja kwa moja na kwenda kukaa langoni kwenye nafasi yake.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.