Mlinzi wa kulia wa klabu ya Singida Black Stars kutoka mkoani Singida, Ande Kofie Cirille raia wa Ivory Coast, anatarajia kukaa nje ya uwanja kwa wiki takribani sita hadi kurejea tena kwenye uwanja kuipambania timu hiyo. Daktari wa timu amethibitisha.
Cirille alipata majeraha hayo katika mchezo wa Nusu Fainali michuano ya Mapinduzi Cup huko visiwani Zanzibar dhidi ya Yanga ambapo alisukumwa na Mlinzi wa kushoto wa Yanga Chadrack Boka na kuangukia upande wa bega hilo kwa nguvu kiasi cha kushindwa kurejea uwanjani kuendelea na mchezo.

Taarifa hiyo imethibitishwa na mganga mkuu wa klabu hiyo Dkt. Shami Shonde katika mazoezi ya kwanza ya timu hiyo baada ya mashindano ya Mapinduzi yaliyofanyika katika viwanja vya shule ya Sheria pale Mawasiliano jijini Dar es salaam.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Katika maelezo yake Dkt. Shonde amesema, nyota huyo hatofanya mazoezi na wenzake kwa wiki mbili kisha atahitaji wiki nne au tatu za kufanya mazoezi na wenzake ili aweze kuimalika na kurejea dimbani.


