Klabu ya West Ham imetoa taarifa rasmi kuhusu kocha wao David Moyes ambaye amesaini mkataba mpya wa kuhudumu klabu hiyo kwa miaka mitatu zaidi.
“Tunafurahi kutangaza kuwa kocha David Moyes amesaini mkataba wa miaka mitatu na timu”, ilisomeka taarifa katika ukurasa wao wa Instagram.
Baada ya kusaini mkataba huo, David Moyes alieleza kuwa West Ham ni klabu kubwa kama alivyosema mara zote. Huku akisifia sana mashabiki wenye moyo na uwanja mzuri ambapo yeye akiwa kama kocha hapo basi atasaidia timu kukua na kufanikiwa.
Msimu wa 2020/2021 ulikuwa wenye mafanikio sana kwa West ham huku wakimaliza nafasi ya 6 katika msimamo wa Ligi kuu ya EPL, kitendo kilichowahakikisha nafasi ya kucheza Europa League msimu wa 2021/2022.
David Moyes anadai kuwa kusalia West ham kwa misimu mitatu zaidi kutasaidia yeye kufanya awezavyo ili kuweka rekodi mpya kwa klabu hiyo.
Chukua namba yako ya akaunti na kiasi cha pesa unachotaka kuweka, sogea kwenye duka lolote la Meridianbet lililo karibu nawe utasaidiwa kuweka pesa.



Sauda
Abaki tu
magdalena
Safi sana
Sarah
Safi sana
Issa
Safi