Baada ya kurejea kutoka katika majukumu ya kimataifa, Federico Gatti anaripotiwa kuweka saini kwenye mkataba mpya wa muda mrefu na Juventus.
Beki huyo wa kati wa Kiitaliano mwenye umri wa miaka 25 amepata hali ya juu na chini tangu ajiunge na Bibi Kikongwe mwaka jana, na kujitengenezea nafasi kwenye kikosi cha kwanza na kufunga bao lake la kwanza la Serie A, lakini pia kuwa mtu wa masihara baada ya bao lake la kujifunga mwenyewe katika kipigo cha hivi majuzi kwa Sassuolo.
Aviator, poker, Roullette, Wild Icy Fruits, Piggy Party na mingine kibao upige pesa na Meridianbet. Ingia www. meridianbet.co.tz.
Gatti amethibitisha kuwa ni beki wa kati mwenye nguvu wa Juventus na amecheza vyema chini ya Massimiliano Allegri msimu huu, akitumia dakika 468 za kucheza katika mechi sita. Kazi yake ilimfanya aitwe kwenye kikosi cha Italia cha Luciano Spalletti kwa mapumziko haya ya kimataifa.
Kama ilivyoripotiwa na Tuttosport kupitia TMW, hatimaye Gatti yuko tayari kusaini mkataba wake mpya na Juventus na ataweka bayana baada ya kurejea kutoka kwenye majukumu ya kimataifa.
Beti na Meridianbet kwa odds kubwa na machaguo kibao, pia unaweza kubashiri mubashara.

Mkataba wake mpya, ambao utakuwa wa mrefu wa kukaa hadi Juni 2028, mshahara wake utapanda hadi takriban Euro milioni 1.5 kwa msimu pamoja na nyongeza. Kwa sasa anapokea jumla ya Euro milioni 1, mmoja wa wachezaji wanaolipwa pesa kidogo zaidi kikosini.