Milan Wamefufua Nia ya Kumnunua Ziyech

Klabu ya AC Milan wana nia na hamu kubwa ya kumnunua winga wa Chelsea Hakim Ziyech  baada ya kufuzu kwa hatua ya mtoano ya Ligi ya Mabingwa hapo jana baada ya kumtandika FC Salzburg.

 

Milan Wamefufua Nia ya Kumnunua Ziyech

The Rossoneri walikuwa na nia ya kumchukua winga huyo wa Morocco mwenye umri wa miaka 29 katika dirisha la usajili la majira ya kiangazi lakini hatimaye walielekeza nguvu zao kwa kipa wa Ubelgiji Charles De Ketelaere, ambaye alisajiliwa kutoka Club Brugge.

Ziyech bado anapata wakati mgumu kupata namba katika kikosi cha kwanza huko Darajani  baada ya kuanza Ligi Kuu ya Uingereza  mara ya mwisho mnamo Agosti na hata sasa ujio wa Graham Potter.

Kama ilivyoripotiwa na Daniele Longo wa Calciomercato.com, Ziyech anapenda kujiunga kujiunga na Milan na wasaidizi wake wameelezea haya kwa wakurugenzi Paolo Maldini na Frederic Massara katika siku za hivi karibuni.

Milan Wamefufua Nia ya Kumnunua Ziyech

Wazo la sasa ni mkataba wa mkopo na chaguo la kununua lililoambatanishwa na Milan wanazingatia kwa dhati operesheni hiyo, ingawa hakuna uamuzi wa mwisho ambao umefanywa.

Milan wanatarajia kuchukua wachezaji wawili wa kiwango cha juu mnamo Januari wanapopigana na Napoli kwa Scudetto, lakini ikiwa tu watafaa mfumo wa Stefano Pioli katika mji mkuu wa Lombardy.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.