Guardiola Avunja Rekodi ya Magoli EPL.

Meneja wa Klabu ya Manchester City, Pep Guardiola amevunja rekodi katika Ligi ya Primier baada ya kuwa meneja wa kwanza kufikisha magoli 500 kwa haraka zaidi akiwa na klabu moja.

 

Guardiola aliiongoza Manchester City hapo jana katika mchezo wa Ligi kuu na kuibamiza Leeds kwa goli 7-0 katika uwanja wao wa nyumbani wa Etihad.

Magoli ya Man City yalifungwa na Kelvin De Bruyne (32′ na 62′) aliyefunga mara mbili, Phili Foden (08‘), Jack Greash(13′), Riyad Mahrez(49′), John Stones(74′) pamoja na Nathan Ake(78’).

Goli la ufunguzi la Foden lilikuwa ndio goli la 500 kwa meneja Pep Guardiola katika mechi 207 akiwa na Man city na kuwa meneja wa kwanza kufikisha magoli 500 haraka zaidi.

Aliyekuwa anashikilia rekodi hiyo ni meneja wa Liverpool, Jurgen Klopp aliyefanikiwa kufikisha magoli 500 katika mechi 234 na sasa akisimama katika nafasi ya pili.


ANZA MSIMU WA SIKUKUU NA BURST THE BANK

Fanya wiki yako iwe ya ushindi mkubwa ndani ya kasino za mtandaoni za meridianbet. Mchezo wa BURST THE BANK🔥🤑 ni moja kati ya mchezo pendwa unaowapa wachezaji mamilioni kila siku. Kwa dau dogo unashinda zaidi.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.