Sababu Kwa nini Paul Pogba Hatakiwi Barcelona?

Taarifa za chini ya kapeti zinadai kuwa raisi wa Barcelona, Joan Laporta amekataa kumsajili nyota wa Mashetani Wekundu, Paul Pogba baada katika mazungumzo yake na wakala wa nyota huyo.

Wakala Mino Raniola na Joan Laporta wanaripotiwa kuwa walipata fursa ya kuonana Jumaane, na wakafanya mazungumzo juu ya biashara za majina kadhaa ya wachezaji, Jina la Paul Pogba pia liliibuka kwenye mazungumzo yao.

Nyota huyo wa Ufaransa anatazamia kuwa mchezaji huru msimu ujao wa joto, wakati mkataba wake wa sasa ukiwa ukingoni.

Paul Pogba
Paul Pogba
Licha ya ugumu wa swali la uwezo wa Barcelona kufikia gharama ya mshahara wa Paul Pogba, Barca wanaonekana kuwa hawana kabisa mpango naye.

Kwa mujibu wa chapisho la kihispania la Sport Laporta ametajwa kuwa amemwambia Mino Raniola kuwa Paul Pogba hatakiwi Camp Nou.

Sababu kubwa inayotajwa ni kuwa Barca hawaoni kama anafaa kwenye aina ya kiungo ambaye kocha mkuu Xavi Hernandez anamuhitaji. Kwa mujibu wa Bosi huyo, Xavi anahitaji kiungo mwenye umbo la kawaida mwenye ufundi zaidi kuliko matumizi ya mwili.

Pogba licha ya ufundi aliojaliwa, pia hutumia nguvu zaidi mchezoni, na Xavi anahitaji kitu tofauti hivyo staa huyu hakidhi vigezo vya Xavi Hernandez.


ANZA MSIMU WA SIKUKUU NA BURST THE BANK

Fanya wiki yako iwe ya ushindi mkubwa ndani ya kasino za mtandaoni za meridianbet. Mchezo wa BURST THE BANK🔥🤑 ni moja kati ya mchezo pendwa unaowapa wachezaji mamilioni kila siku. Kwa dau dogo unashinda zaidi.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.