Hazard Amka Tayari Kumekucha

Tupo katika zama ambazo, Lionel Messi hayupo katika orodha ya wafungaji bora Ulaya. Ni zama hizi ambazo Cristiano Ronaldo ameshindwa kuchukua kiatu cha mfungaji bora wa Serie A kwa misimu miwili mfululizo. Ni zama hizi ambazo Kylian Mbappe na Erling Halland hawashikiki sokoni. Ni zama hizi ambazo dunia inawaweka Alphonso Davies na Trent Alexander-Arnold juu ya Marcelo. Zama zimeenda wapi?

Trent Alexander Arnold

Ninapowaza hivi, ndio ninaamini zama zimebadilika. Muda umebadilika na dunia siyo ile tena. Siyo ile tena ya Lionel Messi kufananishwa na miungu na Ronaldo kuaminika alitengenezwa maabara. Dunia siyo ile tena. Dunia ya sasa ni hii ya Sadio Mane, Mohamed Salah na Kelvin De Bruyne. Ndiyo dunia yao hii. Walisubiri kaka zao wapite. Sasa ni zamu yao kutamba.

Ila yupo wapi Eden Hazard? Yule aliyewapa Chelsea Europa pale Baku. Yule aliyewanyima Tottenham ubingwa. Yule Hazard aliyewakokota Arsenal umbali wa mita 50 kisha akawatungua. Ameenda wapi? Yule mchezaji bora wa epl mwaka 2015. Nani anajua alipo?

Mara ya mwisho alionekana akisajiliwa Real Madrid kwa pauni 100 milioni. Kila mtu aliridhika na lile dau. Hakuna aliyekuwa na mashaka. Hata uso wa Perez haukuwa na wasiwasi, ile siku anamtambulisha mbele ya mashabiki wa Real Madrid pale Santiago Bernabeu. Alishindwa tu kuwaambia kuwa nimemleta mrithi wa Ronaldo. Ila moyoni mwake alijua hivyo. Hata mashabiki jukwaani walijua hivyo. Wakamkabidhi jezi namba 7.

Nyuma aliwaacha mashabiki wa Chelsea na majonzi makubwa moyoni. Ila waliridhika kwa yale aliyowafanyia. Wakiamini anaenda kupata mafanikio ambayo asingeyapata kwao. Zaidi ya yote, Hazard alikuwa anaenda kuichezea timu ya ndoto zake. Isitoshe, alikuwa anaenda kufanya kazi na shujaa wake. Zinedine Zidane. Mtu aliyemfanya aupende mchezo wa soka.

Ila msimu sasa umeondoka. Hazard hajawa yule Ronaldo Real Madrid waliomdhania. Amefunga bao moja na kutoa assit 4 msimu mzima. Huyu siyo Hazard aliyemnyima Mourinho usingizi. Siyo Hazard aliyeitwa mchezaji bora baada ya Messi na Pep Guardiola. Huko ulipo Eden, tafadhali rudi maana dunia bado imelala inakusubiri uiamshe.


Umekuwa mteja muaminifu wa meridianbet? Basi fahamu kuwa kuna zawadi kibao hadi 5% ya pesa yako inarejeshwa kwako. Kila wiki unaweza kurudishiwa mpaka Tsh 250,000.

Soma zaidi

43 Komentara

    Good news
    @meridianbettz

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Hazard amebadilika sana, Ni wa leo siyo wa jana.

    Jibu

    Kwa kipindi majina aya mawili ya messi na ronaldo yamevuma kwa kipindi kirefu katika medani ya soka

    Jibu

    Yeah! nikweli Hazard wa jana si waleo,
    But ikumbukwe sio kila siku ijumaa.

    Jibu

    Zama zao zimeshakwisha Ronaldo na messi wachezaji chipukizi wamekua na molali sana sikuizi

    Jibu

    Kila kitu kina mwisho wake zama zao zimeisha sasa zamu ya wengine mess na Ronald wakae pembeni

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Nice

    Jibu

    Kweli kabisa tarehe ,mwezi na mwaka hata siku zinabadilika hakuna sasa wale ambao walikuwa wanajulikana kwa kupokezana vijiti sasa wamekaa pembeni wamewapisha wadogo zao au wamejisahau na kuridhika walicho kipata tunashindwa kuelewa mashabiki.

    Jibu

    Maoni:kwel zama zinabadilika kabisa

    Jibu

    Goodupdate#meridianbet

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    ronaldo na messi watulie sasa ni zamu ya wenzao

    Jibu

    Hazardi jembe

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Kila jambo na wakati wake#Meridianbettz

    Jibu

    Gud news

    Jibu

    kweli zama zimebadilika

    Jibu

    Kupata mafanikio ktk timu moja ni jambo jingine ktk timu nyingine kwenye mfumo tofauti na Kocha tofauti. Naamini Hazard atapata mafanikio endapo atapata nafasi ya kucheza na kupona majeruhi vizuri#meridianbettz

    Jibu

    Habari njemaaa

    Jibu

    Siku hazigandi Maendeleo ndio yanayotakiwa!!!

    Jibu

    Good news

    Jibu

    habari njema#meridianbettz

    Jibu

    Hazard ni mchezaji mzuri Sana

    Jibu

    Habari nzuri

    Jibu

    Hazard yuko vzur sana tatizo mfumo wa uchezaji wa Madrid auwez n wakichoyo na wakujuana na ndo maaana hata CR 7 ulimshinda kabisa

    Jibu

    Hazard anaitaji muda,ila naamini msimu ujao ataweza kufanya vyema.

    Jibu

    Hazard upepo umemkataa hispania

    Jibu

    Hazard ni msimu mbaya kwake sana ila apambane muda anao

    Jibu

    Matatzo tu akupenda

    Jibu

    Kila Jambo na wakati wake

    Jibu

    Huu sio msimu mzuri kwa Hazard

    Jibu

    Zama zimebadirika cr7 na messi wanazeeka

    Jibu

    Hazard anahitaji muda,ila naamini msimu ujao ataweza kufanya vizuri zaidi.

    Jibu

    Kweli kila majira yana matukio yake hazard sasa ni zamu yake#meridianbett

    Jibu

    Kwa kipindi majina aya mawili ya messi na ronaldo yamevuma kwa kipindi kirefu katika medani ya soka inabidi akaze achukue nafasi zaoo

    Jibu

    Zama zinaenda na nguvu pia zinapungua sasa n muda wa vijana

    Jibu

    Ni jambo zuri sana kuona kwamba kuna wachezaji wengine ambao walikua na kiu ya kuwa kama messi na Ronaldo ni jambo la kifurahisha sana hata wao wenyewe watakua wanajidai mnoo

    Jibu

    Dah kweli maisha yanabadilika

    Jibu

    Kila nyakati zina mda wake kwa sasa messi na ronaldo ndio mwisho wao.

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Gud update

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.