Inter Vs Shakhtar:
Kocha wa Inter, Antonio Conte anaonekana anataka kukipa kikosi chake kile kile kutia kazi kwenye gemu dhidi ya Shakhtar Donetsk, wakati Christian Eriksen akipigwa benchi tena.
Ni nusu fainali ya Ligi ya Europa Inter Vs Shakhtar, itaanza saa 4.00 usiku.
Timu hizi zote zimeonesha uwezo mkubwa katika safari yake ya Ligi ya Europa. Mshindi wa mechi hii atakutana na Seviila ambao wametoka kumchapa Man United bao 2-1.
Danilo D’Ambrosio anaendelea kufanya vizuri Inter akimsubirisha benchi Antonio Candreva. Wakati Alexis Sanchez pia hayupo, Romelu Lukaku na Lautaro Martin watasimika safu ya ushambuliaji.
Diego Godin, Stefan de Vrij na Alessandro Bastoni wameandaliwa kuendelea kuwepo kwenye safu makini ya ulinzi, wakiwa wametoka mapumzikoni kwa takribani siku 6. Wakati huo Ashley Young atapatikana upande wa kushoto, na Nicolò Barella, Marcelo Brozovic na Roberto Gagliardini akishikilia dimba katikati.
Shakhtar Donetsk wanatarajia kutimba na mfumo wao wa kawaida wa 4-2-3-1, ambapo Junior Moraes atakuwa ndiye kila kitu kwenye mashambuli.
David Khocholava na mtoto machachari Valeriy Bondar wanatarajiwa kupambania nafasi kwenye safu ya ulinzi, huku, Marlos, Alan Patrick na Taison wakionekana tayari wana nafasi nyuma ya Junior Moraes.
Inter Vs Shakhtar: Vikosi Vinavyotarajiwa
Inter : Handanovic; Godin, De Vrij, Bastoni; D’Ambrosio, Barella, Brozovic, Gagliardini, mchanga; Lukaku, Lautaro
Benchi: Padelli, Ranocchia, Skriniar, Biraghi, Candreva, Musa, Sensi, Borja Valero, Eriksen, Agoume, Esposito
Shakhtar: Pyatov; Dodo, Krivstov, Khocholava, Matvyenko; Marcos Antonio, Stepanenko; Marlos, Alan Patrick, Taison; Kijana Moraes
Benchi: Turbin, Vitao, Fernando, Dentinho, Marquinhos Cipriano, Bondar, Konoplyanka, Maycon, Kovalenco, Solomon, Bolbat, Tete
Drops and Wins!
Umeijua hii? Ni promosheni kabambe ya ushindi kwenye Casino ya mtandaoni ya Meridianbet! Unaweza kushinda hadi Euro 2,000,000 leo.


felister
vikosi vimetulia
Shafii
Hii mechi wadau wa soka tunaisubilia Sana kwa hamu.
Zeiyana
Inter wanakua na mototo wa kuotea mbali subiri tuone matokea
Janeflora malisa
Iko vzr
Genia Sikaluzwe
Imekaa poa San
Lydia Emmanuel Magoti
Hii mechi tunaisubili kwahamu apatoshi hapo
Sadick
Inter ina kikosi cha ushindi,tusubiri dakika 90#meridianbettz
Povel
Vikosi vipo POA sana Ila mpr dk 90
Hope mwaikuka
Hii mechi cjui itakuaje
Furahav
Leo hatumwi mtt dukani.
Devotha
Vikosi viko poa ngoja tuone nani mshindi
JULIANA
Langu jicho mwe!
Sabrina
Vikosi vipo vizuri tunasubiri kuona kabumbu
Gabriel
Mech kal sana 👍
Asia Abdy
Inter ana nafas kubwa ya ku win
Dorophina
Inter inakikosi kizuri sana tunasubilia mpaka mwisho wa mchezo
Nasra
Vikosi vipo vzuri
Sauda
Iko poa sana
Flomena
David Khocholava na mtoto machachari Valeriy Bondar wanatarajiwa kupambania nafasi kwenye safu ya ulinzi, huku, Marlos, Alan Patrick na Taison wakionekana tayari wana nafasi nyuma ya Junior Moraes.
aisha
Inter wako vizuri ushindi kwao ni lazima jamani tusubili tuu tuone
Ester jackson
Inter walipanga kikosi vizuri mpaka kupelekea ushindi
Caroline
Asante meridianbet Kwa taarifa
Tatu
Hapo wababe wamekutana
Salma ngende
Vikosi vmetulia
farida ahmadi
Mechi kalii Sana hizi si yakukosa kabisah
Saupha mohamed
Vikosi vipo vizuri
Samiah
Safi
Latifa juma mohamed
Mechi ilikuwa kali Sana
David Pere
Inter walistahili ushindiii
Omary lukumbi
Inter walistahili kupata matokeo tuu
warda
Niliikosa hii