Ishu Ya Inonga Kuja Yanga Imekaa Hivi

Habari kutoka Yanga, zinasema tayari mabosi wa klabu hiyo wameanzisha mazungumzo na FAR Rabat ya Morocco ili kuona kama kuna uwezekano wa kuipata saini ya beki Inonga Bakka.

 

Ishu Ya Inonga Kuja Yanga Imekaa Hivi

Na hiyo ni kwa vile bado ana mkataba wa Mwaka mmoja na kikosi hicho kilichomsajili mwanzoni mwa msimu huu kutoka Simba.

Beki huyo wa kimataifa wa DR Congo, anapigiwa hesabu za kutua Yanga kuongeza nguvu eneo la ulinzi la kati linaloongozwa na Dickson Job na Ibrahim Hamad ‘Bacca’ na Bakari Mwamnyeto ambaye amekuwa hapati nafasi kubwa ya kucheza.

Chanzo cha habari Hii kilisema: “Yanga ina uhitaji mkubwa wa kusajili mchezaji wa eneo hilo. Ila kuhusu nani anakuja ni mapema kuzungumza kwa sasa, lakini mchakato unaendelea na majina ya wachezaji wanaotazamwa kwa ajili ya kuongeza nguvu eneo hilo yapo mezani na tayari yameanza kufanyiwa mchakato na jina la Inonga ni miongoni mwao,”

Ishu Ya Inonga Kuja Yanga Imekaa Hivi

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Chanzo hicho kiliongeza kuwa mchakato wa kutafutwa kwa beki huyo ulianza baada ya kuachana na Gift Fred kutoka Uganda na tangu hapo Yanga wamekuwa na wakati mgumu kupata mchezaji ambaye ataweza kuendana na ushindani uliopo hasa kwenye eneo hilo.

 

Ishu Ya Inonga Kuja Yanga Imekaa Hivi

Inonga amekuwa beki tegemeo kwa sasa wa kikosi cha AS FAR Rabat, kilichoondolewa katika hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa kufungwa na Pyramids ya Misri kwa jumla ya mabao 4-3 baada ya awali kufungwa 4-1 ugenini na kuja kushinda nyumbani mabao 2-0.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.