Juma Abdul, Utarudi Lini?

Miaka ya 1990s John CruyfF’ aliabudu sana mfumo wa tiki taka na umiliki wa mpira kwa vijana wa La Masia pale barcelona, na ndipo soka likalipa fadhila kwa kumtunuku dunia ya kulia beki wake wa kulia ALBERT FERRER, akawa mtu na nusu.

Ferrer aliyaishi maajabu yake ya mguu wa kulia , alimwaga cross zilizompa magoli Ronald koeman na mwenzake Angel Nadal , muda huo hata Dani alves hakudhani kama ipo siku angevaa uzi wa barca kwani Dani alves hakufanya hata robo ya alichokifanya ferrer kwenye dunia ya kulia ya fc barca.

Miaka ya 2015 jina la Juma Abdul Mnyamani lilitawala sana masikioni mwa wengi, binafsi nilikufananisha na Henry mcKop beki wa Zimbabwe kongwe iliyocheza World Cup.

Wengi wakakushindanisha na Shomari Kapombe, Juma uliyamwaga maji kwa Donald Ngoma, Hamisi Tambwe na Simon Msuva, na kazi ya kufunga ikawa rahisi sana, tangu hapo moyo wangu ukazama kwako.

Nikaanza kustaajabu nilipomuona Paul Godfrey boxer akikuweka benchi hadi timu ya taifa, hapa ndipo dhambi ya usaliti ilipoanzia juma ,licha ya majeruhi ya muda mrefu ya kapombe, Juma bado haukutuita, nafasi bado ipo Juma, tufikirie na sisi, bado tunaihitaji huduma yako pale kwa Mkapa.

Kila nikitazama ile Yanga ya kampa kampa tena, huku Msuva pale Ngoma, katikati Kamussoko mbele yake Tambwe, kushoto Oscar Joshua, kulia nilikuwa nakona wewe, zile krosi zako zikanipeleka kijijini Novo Hamburgo nchini Brazil, mahala alipozaliwa beki wa kulia Maicon Douglas sessinado. Sikuchoka kukutazama.

Moyo wangu umejaa makelele ya lawama za wapenda soka, ningefurahi kumuona Kibwana Shomari anapata uzoefu kwako, kama anavyoupata Duchu kwa kapombe pale simba. Mitaa imekumiss Juma, unarudi lini?

Kuna vitu Ligi yetu inakosa kutoka kwako. Nimewaza zile cross zako angezikuta Michael Sarpong, zile V- pass zako zingemkuta Yacoba, na zile pass za Carlinho zingekufikia wewe, daaaaah, Jumaa, Ipunguze hii dhulma, tumeimiss ile ladha ya chocolate ya miguu yako.


UMEJARIBU HII POKER YA VIDEO?

Jaribu sasa hapa Meridianbet. Ukiacha ukweli kuwa itakupa burudani maridadi, bado inakuhakikishia ushindi mkubwa. Kazi kwako kukusanya ushindi!

Meridianbet Casino

INGIA MCHEZONI!

22 Komentara

    Juma Abdul ni mmoja ya wachezaj wa beki ya kulia wanaoitendeah haki namba hyo natuamain hatafany vzr Zaid na kuvuka mipaka ya nje kwa uwezo anamkubwa wa kusaka kabumbu kila la kheri juma Abdul Mnyamani

    Jibu

    Ni makini sana kwa timu kama hii

    Jibu

    Anajituma sana ni mchezaji wa viwango vya juu

    Jibu

    Dah ! Hii story imeishaje sasa

    Jibu

    Daah hatari sana

    Jibu

    Asante kwa taarifa meridianbet

    Jibu

    labda kuna vitu tu vimeingiliana juu yake lakini bado juma abdul hajashuka viwango vyake kila la kheri mpambanaji

    Jibu

    Anajitahidi sana

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Anajituma Sana na kujituma akiwa uwanjani

    Jibu

    juma abdul katika kuucheza mpira anajua sana wampange tu vizuri atarudi

    Jibu

    Good update

    Jibu

    Nice

    Jibu

    Kijana yupo makini Sana anajituma sana

    Jibu

    Habari njema sana

    Jibu

    Ni mchezaji mwenye kiwango anajituma sana

    Jibu

    Beki makin sana moja ya mabek bora ligi ya tanzania

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Juma Abdul ni mmoja ya wachezaj wa beki ya kulia wanaoitendeah haki namba hyo natuamain hatafany vzr Zaid na kuvuka mipaka ya nje kwa uwezo anamkubwa wa kusaka kabumbu kila la kheri juma Abdul Mnyamani

    Jibu

    Juma yupo vizuri sana

    Jibu

    Ni makini sana kwa team kama hii

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.