Juventus wanatajwa kuwa tayari kumuuza kiungo Aaron Ramsey msimu huu wa joto, baada ya sintofahamu ya hatma ya staa huyo.
Ramsey kwa sasa yupo mazoezini na kikosi cha Ureno kuelekea mechi za kimataifa za European Championship baada ya kucheza mechi 30 akiwa Juventus.
Nyota huyu wa miaka 30 hakuwepo kwenye kikosi cha cha Pirlo kilichocheza mechi sita zilizopita za Serie A, pia alikosa Mechi dhidi ya Wales kwa sababu ya changamoto ya jeraha.
Kwa mujibu wa Calciomercato, Juventus wanatarajia kumuuza Ramsey msimu wa joto wakitaka kufanya mabadiliko makubwa kikosini hapo baada ya kushindwa kutetea ubingwa wa Serie A.
Ramsey amekuwa akihusishwa na kurejea tena Barcelona. baada ya Arsenal kutajwa ikimuhitaji kwa mara nyingine, ambako alikuwepo kwa takribani miaka 11 kati ya 2008-2019, pia Liverpool.
Tangia kiungo huyu awasili Turin kutoka Arsenal, amefanikiwa kupata magoli sita tu na kutoa usaidizi kwa wa magoli kwenye mechi 65 alizocheza akiwa na Juve, na mkataba wake na Juve unafika mwisho 2023.
BONASI YA 50% KILA SIKU KATIKA KASINO ZA EVOPLAY HAPA MERIDIANBET.
Meridianbet na Evoplay Kasino wanakupa bonasi ya 50% ya kiasi utakachoweka katika akaunti yako leo. Unasubiri nini ni wakati wa kupiga pesa sasa na Mabingwa.
Wamuuze Ramsey wamnunue Pogba
Wamuache
Wamuache
Wamuuze