Meneja wa Chelsea, Thomas Tuchel amethibitisha wachezaji wake N’golo Kante na Thiago Silva wamepatikana na maambukizi ya Covid-19 ndio maana walikosa mchezo wa hapo jana.

Kante na Silva walikosa mchezo wa kwanza wa nusu fainali ya Carabao baina ya Chelsea dhidi ya Tottenham ambapo waliibuka na ushindi wa 2-0 katika uwanja wa Stamford Bridge.
“Ndio, bahati mbaya Thiago silva ba N’Golo Kante” alisema Tuchel endapo kuna wachezaji walioripotiwa kuwa na maambukizi ya Covid-19.
“Ni kubwa kwetu kwasababu ni wachezaji wakubwa. Tumepata taarifa leo asubuhi [jana], ni changamoto, lakini tutajaribu. Wachezaji wote waliopo tunawaamini.
“Tutawahimiza mpaka mwisho. Hali haijabadilika tangu wiki kadhaa nyuma, si wakati wa kurejea, kuanzaia hapa tunaangalia utatuzi. Nina imani na wachezaji watakao cheza natumaini wataonyesha kiwango bora.” aliongeza Tuchel.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.


