Luis Nani ni jina lenye heshima kubwa miongoni mwa majina ya wachezaji waliowahi kuitumikia Manchester United. Nani ni mchezaji aliyerithi mikoba ya Cristiano Ronaldo na aliitendea haki kwa nafasi yake.
Mwaka 2008 wakati ambapo Man United walibeba kombe la Ligi ya Mabingwa, Luis Nani alikuwa miongoni mwa wachezaji waliopeleka mafanikio hayo Old Trafford, hii inakwenda sambamba na makombe mengine mengi aliyoyapata akiwa na Man United.
Nani aliwahi kucheza timu moja (Sporting Lisbon) na Bruno Fernandes kwa msimu mmoja – 2018/19 kabla hajatimikia Marekani ambapo anaichezea timu ya Orlando City mpaka sasa.
Alipokuwa Sporting, Nani aliwahi kumshauri Fernandes kujiunga na EPL tena kama atapata nafasi ya kujiunga na Manchester United basi asifanye makosa, aitumie nafasi hiyo. Fernandes alifanya kweli mwezi Januari, 2020 na kuanzia hapo imekuwa ni safari ya mafaniko kwake.
Mpaka sasa, Fernandes amehusika kwenye magoli 34 ya United – amefunga 21 na kutoa pasi 13 za magoli. Takwimu zinaonesha, hakuna mchezaji yeyote kwenye mpira wa Uingereza aliyehusika kwenye magoli mengi kumzidi Bruno (Kane 31, Son 25, de Bryune 23 na Salah 22) tangu alipojiunga na EPL mwezi Januari.
Akizungumza na United Review, Luis Nani ameshangazwa na uwezo wa Man United kwa kipindi kifupi alichokuepo kwenye timu hiyo.
Luis Nani anasema ” miaka kadhaa iliyopita nilimpa ushauri Bruno Fernandes, wakati ule nilikuwa nikicheza naye Sporting Lisbon. Bruno kwa sasa ni mchezaji mzuri zaidi kuliko kipindi ambacho tulikuwa tunacheza pamoja. Alikuwa anafanya vizuri kwenye Ligi ya Ureno – lakini Ligi ya Ureno sio sawa na Premier League, kwenye kila kitu kunaugumu na ubora mkubwa.
“Niliuona uwezo mkubwa kwa Bruno na nilimshauri aende Uingereza kama atafikiria kubadilisha ligi. Nilimwambia , ‘Uchezaji wako utafaa sana kule na mashabiki watapagawa na uwezo wako’
“Aina ya uchezaji wake ni kitu ambacho mashabiki wanakikubali. Ni mchezaji ambaye anapenda kuchukua maamuzi magumu, anabeba majukumu kwenye mchezo, anatoa pasi ngumu na kupiga mashuti. Haogopi kufanya makosa, anafikiria mafanikio na kuifanya timu ifanikiwe. Anajua faida ya kufanya hivyo, hiyo ndio Man United.
“Bruno amefanya makubwa sana mpaka sasa, amefunga na kutengeneza magoli mengi lakini ninadhani ataendelea kuwa bora zaidi na kuisaidia timu kupata mafanikio zaidi.”
Hadi 130,000,000 TSH Kutolewa kwa washiriki wa shindano la Playson Cashfall. Unaipata kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet Pekee. Jisajili sasa, kisha ingia mchezoni kabla ya Novemba 29.
aisha
Namkubali sana kijana
David Pere
Bruno amefanya makubwa sana mpaka sasa, amefunga na kutengeneza magoli mengi lakini ninadhani ataendelea kuwa bora zaidi na kuisaidia timu kupata mafanikio zaidi
Genia Sikaluzwe
Kiukweli yuko vizuri Sana
Lydia Emmanuel Magoti
Yupo vizuri kijana anajua mpila Fernandes mpambanaji
Hopemwaikuka
Nani namuelewaga sana
Adelta
Luis nani anakubalika sana
Caroline
Luis anaongea kweli
Fatina mfingi
Luis yuko vizur sanaa anajua anacho kifany
Tatu
Kijana yupo vizuri
Fatuma kasomo
Yupo vizuri
Magdalena
Fernandes ni kijana makini
Saupha mohamed
Jamaa yupo vizurii
Dorophina
Fernandes yupo vizuri sana akiwa uwanjani anajituma sana
Rahma
Kijana Yuko poa
Sauda
Anajituma sana
warda
Sijamuona mda mrefu NANI