Mama mzazi wa nyota wa PSG, Kylian Mbappe, Fayza Lamary amekanusha madai kwamba mshambuliaji huyo amekubali kuongeza muda wake wa kusalia katika klabu hiyo ya Ufaransa.

Mustakabali wa kinda huyo umekuwa mjadala katika msimu mzima, huku mkataba wake wa sasa na mabingwa hao wa Ufaransa ukitarajiwa kukamilika mwezi Juni.
Hii inamaanisha kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 atakuwa mchezaji huru, na kuhamia Real Madrid, ambao wamemfuatilia kwa muda sasa.
Klabu hiyo ya Ufaransa hata hivyo imeongeza juhudi za kumshawishi Mbappe kusaini mkataba mpya, lakini hakuna kilichoafikiwa.
“HAKUNA makubaliano ya msingi na Paris Saint-Germain au klabu nyingine yoyote,
Majadiliano kuhusu mustakabali wa Kylian yanaendelea kwa utulivu mkubwa ili kumruhusu kufanya chaguo bora zaidi, kwa heshima ya pande zote”. Mama mzazi wa Mbappe amesema.-
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.