Bosi wa Atletico Madrid, Diego Simeone tayari ameshaanza kuandaa mpango kwa ajili ya kulinda taji msimu wa 2021-22. Taarifa zinataja kuwa Lautaro Martinez yupo kwenye mipango yake.
Baada ya kuwaa ubingwa na Atletico Madrid kwa mara ya kwanza tangia mwaka 2014, nguvu yote sasa inaelekezwa kwenye mipango ya kuwa bora zaidi msimu ujao.
Nyongeza ya mkataba wa Diego Simeone imekuwa kipaumbele cha klabu, huku mkataba wake wa sasa ukiwa unafika tamati9 mwisho wa msimu ujao.
Ripoti zinataja kuwa meneja huyu yupo mbioni kusaini mkataba mpya ambao utamshuhudia akisalia klabuni hapo hadi mwishoni mwa msimu wa mwaka 2023/24.
Ukiacha swala la mkataba wake, Simeone anatarajiwa kufanya makubwa kwenye dirisha la usajili la msimu huu wa joto, na kwa mujibu wa ripoti za Diario AS, Lautaro Martinez ni mmoja wa kipaumbele chake kutoka Milan.
Martinez alikuwa anahusishwa na uhamisho wa kwenda Barcelona, lakini Barca wanaonekana kuwa na vipaumbele tofauti hivyo Atletico Madrid wamaweza kuwa kwenye nafasi nzuri zaidi.
Chukua namba yako ya akaunti na kiasi cha pesa unachotaka kuweka, sogea kwenye duka lolote la Meridianbet lililo karibu nawe utasaidiwa kuweka pesa.
dorophina
Nice update