Mchambuzi wa soka nchini, Ally Mayay amesema ana uzoefu na dabi, amesimulia namna zamani walivyokuwa wanaandaliwa kuelekea mchezo huo na asili ya ushindani ulivyo baina ya klabu hizo.

“Zamani kama wachezaji tulikuwa tunadai, viongozi walikuwa wanatulipa kabla ya mechi,tulihamasishwa hilo lilifanya hata kama timu ipo chini ya kiwango, ikiingia uwanjani inakuwa na ushindani mkubwa ambao hauwezi kutabiri nani anaweza akashinda mechi,”amesema Mayay na ameongeza kuwa;

“Kwa jicho la ufundi Simba ipo vizuri kila idara, inacheza kwa kombinesheni, uwezo wa mchezaji mmoja mmoja unaonekana, kocha anaijua timu yake kujua ni jinsi gani ya kubadili matokeo kwa muda wowote, Yanga naiona changamoto kwa Nabi bado hajazoeana na wachezaji wake na bado hana kikosi cha kwanza,”
TENGENEZA FAIDA KUPITIA MCHEZO WA TITAN DICE UKIWA NA MERIDIANBET KASINO
Unapokuwa kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, huna sababu ya kucheza kwa mashaka. Titan Dice, ni mchezo unaweza kukupatia mamilioni kwa mzunguko mmoja!



Amiri Kayera
Lazma afungwe mtu hii hakuna draw
aisha
Lazima kichapo kitembee
Adelta
Tunasubiri tuone itakuwaje ndani ya dakika90
neema hassan
Mtanange wa kibabe
Elika
Mpira wa kibabe huo
Sarah
Mtanange wa nguvu
Lydia Emmanuel Magoti
Mtanange watari huu
Magdalena
Tulikuwa tunasubiri kwa hamu kubwa
Mariam mtandama
Duuuh
Sauda
Lazima mtu achapike
David Pere
Ilitakiwa afe kweli mtu lakini Ndio hivyo tena