Mbappe na Neymar Hawawezi Kuwa Messi na Ronaldo!

Mbappe na Neymar wangekuwa wafalme wapya? Ulimwengu wa soka umeshuhudia kwa mara ya kwanza ndani ya miaka 15, hatua za nusu fainali na fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya zikichezwa bila uwepo wa Lionel Messi na Christiano Ronaldo!

Kipigo cha aibu, 8-2 cha Bayern Munich kwa Barcelona katika hatua ya robo fainali kilihitimisha safari ya Messi kwenda Lisbon huku safari ya Ronaldo ikitamatishwa na Lyon katika hatua ya 16 tu ya mashindano hayo.

Hii inaweza kuwa mwanzo wa mwisho wa ufalme ambao Messi na Ronaldo waliuanzisha katika soka la Ulaya. Wengi tulitazamia kuwa ufalme wa wakali hao ungerithiwa na wakali wengine, Mbappe na Neymar! Lakini baada ya mechi ya jana kati ya timu yao PSG na Bayern Munich inabidi tujiulize tena juu ya hili.

Mbappe na Neymar: Wameshindwa Kuifanya PSG Ibebe UEFA Yao ya Kwanza

Wakati Messi akiwa sehemu ya kikosi kilichobeba UEFA mwaka 2006 dhidi ya Arsenal pale Paris, kuwa mchezaji wa muhimu na alieibeba Barcelona katika ushindi dhidi ya Manchester United mwaka 2009 pale Rome huku akiwa na miaka 19 tu, Kylian Mbappe na Neymar wameshindwa kuipa Paris Saint-Germain ubingwa wake wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa.

Mbappe na Neymar hawakuonesha viwango vya kuridhisha katika fainali hiyo kati yao dhidi ya Bayern Munich, mechi iliyoisha kwa PSG kukubali kipigo cha 1-0!

Mbappe na Neymar wasubiri
Kingsley Coman akishangilia kwa furaha na wachezaji wengine wa Bayern Munich huku akiwa ameshikilia kombe ambalo limepatikana kutokana na goli lake

Wameshindwa Kutumia Nafasi Vizuri

Wote, Mbappe na Neymar walipata nafasi nyingi kipindi cha kwanza ambazo wangezitumia kuongoza mchezo huo lakini hawakufanya hivyo, hata walivyoaminiwa na kocha kuendelea kubaki kipindi cha pili hawakuisaidia timu kusawazisha matokeo kwa timu yao.

Kama Neymar angekua makini, angeiwezesha PSG kupata goli la kuongoza katika dakika ya 18 tu ya mchezo lakini shuti lake dhaifu lilizuiliwa kiurahisi kabisa na Manuel Neuer.

Mbappe nae alipata nafasi adhimu ya kufunga dakika chache kabla ya mapumziko, kocha na benchi zima la ufundi walishasimama kushangilia.

Mashabiki wa PSG kuanzia kule Paris, Lille, Bordeaux na Dar es Salaam, Mbeya mpaka Lindi waliokuwa wanafuatilia mechi kupitia luninga tayari walishaanza kushangili, lakini alichokifanya ni yeye mwenyewe ndo’ anajua! Alichopiga hakina hata hadhi ya kuitwa kijishuti mtoto!

Hata kipindi cha pili baada ya PSG kuwa wanaongozwa kwa goli moja, bado Mbappe na Neymar walishindwa kuonesha ubora wao kuisaidia timu. Dakika za mwisho za mchezo zilishuhudia Neymar akishindwa kufanya maamuzi sahihi akiwa ndani ya eneo la hatari la adui, hakuliona lango wala mwenzie wa kumpasia!

Umri wa Neymar, hapana! Labda Mbappe

Neymar mpaka sasa ana umri wa miaka 28, fainali hii ilikua ni nafasi yake ya pekee kuonesha ubora wake. Kuonesha kwamba anaweza kuwa mrithi wa mmoja kati ya Messi ama Ronaldo. Zaidi kuonesha kuwa anaweza kushinda klabu bingwa nje ya kivuli cha Messi. Kwa kiwango alichokionesha jana, ni wazi kuwa hajayapatia jibu stahili maswali hayo na ubaya ni kuwa tayari anaielekea miaka ya 30s.

Kwa upande wa Kylian Mbappe yeye bado anayo nafasi ya kuwa bora kama magwiji hao, lakini kwa siku ya jana bado hakufanya hivyo. Labda anaweza kusingizia kuwa alitoka kwenye majeraha  ya enka, lakini asisahau kuwa alicheza katika mchezo wa nusu fainali! Mbappe hivi sasa ana miaka 21, bado ana miaka mingi ya kucheza, labda huko mbeleni anaweza kututhibitishia kuwa yeye ni bora kama Messi ama Ronaldo, lakini kwa jana HAPANA!

 


Beti Mbio za Mbwa Mubashara

Hii ni rahisi zaidi! Hapa USHINDI unaupata kwa kuchagua mbwa anayeshinda mbio na machaguo mengine yenye odds tamu.

Cheza Hapa

39 Komentara

    Jamani Mie imeniuma sana PSG kukosa Huu Ubigwa

    Jibu

    neymar na mbappe hawawezi kua Kama Messi na Ronaldo labda uko mbeleni

    Jibu

    Viwango vyao bado hawawezi kumfikia Messi@meridianbettz

    Jibu

    neymar na mbappe wafanye kazi ya ziada mpaka kuwafikia hao

    Jibu

    Maoni:kwel kabisa japokuwa messi na ronaldo ushindani wao umepungua sana tangu ronaldo haondoke kwenda juve

    Jibu

    Bora ajitaidi kuongeza bidii ili amfikie messi

    Jibu

    Kila MTU Jana aliona kabisa huu ushindi wa PSG lakini imekuja kutokea tofauti pale mbappe na neymar alivokuja kucheza vibaya uwanjani na kuzidiwa uwezo na kijana mdogo sana aitwae kingsley coman

    Jibu

    Nikweli Neymar na mbappe awawez kuwa Kama Messi Ila kwakizidisha juhudi Wana weza wakawa kwenye levo ya Messi Ila wakaze tuu Ila Messi ana mpinzani wakae wakijua Messi yupo vizuri

    Jibu

    hata wafanyeje hawawezi kimfikia#meridianbettz

    Jibu

    Messi kile ni kifaa kingine usikifananishe na mtu mwingine

    Jibu

    Awawez kufanana na wengine

    Jibu

    Hawana uwezo wa kuwafikia messi na Ronaldo.

    Jibu

    Kuwafikia mess na Ronaldo wafaye kazi kweli kweli

    Jibu

    Ni wachezaj wazuri sema hawana umakini pia hicho ndio kinawafanya wasifikie levo za mess na ronaldo kwa chans kama zile walizopata na kwa mechi kama ile sidhani kama angeluw mess ama cr7 wangefanya ajiz

    Jibu

    Huu ni ukweli usiofichika kuwa Messi na CR7 ni watu wa level nyingine kabisa dhidi ya Mbappe na Neymar, Messi na CR7 wataendelea kutamba kwenye kizazi hiki adi watakapoacha soka la kulipwa

    Jibu

    Record za Messi na Ronaldo sio rahisi kufikiwa na yeyote kwasasa kwa namna walivyo na shauku ya kupata mafanikio zaidi na zaidi. Jana Neymar na Mbappe haikuwa siku yao#meridianbettz

    Jibu

    neymar na mbappe hawawezi kua Kama Messi na Ronaldo labda uko mbeleni

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Yuko sahihi

    Jibu

    Hayo maneno tu kwn wakiongezeha bidii na kujituma wanawez fika malengo hakuna kukata tamaa kwny kutafuta maisha

    Jibu

    Wamefanya kwa nafas zao ila ndo hvyo lazma tukubaliane na kilichotokea

    Jibu

    Messi na ronaldo izo level nyingine wapambane xana!!!

    Jibu

    Kufk level iz ngum san

    Jibu

    Duuh Huo nie ukweli usio pingika hauwezi kuwafananisha kabisaa

    Jibu

    Messi na ronaldo ni mpango mwengine cha msingi mbape na neymar huu ndo wakati wao kwa sababu messi na ronaldo zama zao zinaenda ukingoni.

    Jibu

    Hayo maneno tu kwn wakiongeza bidii na kujituma wanawez fika malengo hakuna kukata tamaa kwny kutafuta maisha , siku zote mtafutaji hachoki

    Jibu

    Messi na ronaldo ni mpango mwengine cha msingi mbape na neymar huu ndo wakati wao kwa sababu messi na ronaldo zama zao zinaenda ukingoni.

    Jibu

    Kweli kabisah ila wasikate tamaa waendelee kukaza buti neymar na mbape

    Jibu

    Neymar akaze buti

    Jibu

    Kila jambo linawezekana wakiamua kwani hao Messi na Ronaldo wamefanyaje mpaka wamefika hapo walipo

    Jibu

    Wapambane, wataweza

    Jibu

    Ni suala la kuwap muda tyuu vijana wakali

    Jibu

    Tatizo lake mbappe alikua na shauku sana ..!nia yake yeye kuipelekea clabu yake kufuzu ubingwa balani ulaya ili kutimiza ndoto yake alijisahau kama watu mwenyew wanao kutana nao si wamchezo mchezo..!ila sio mbaya bado hana nafasi kubwa tu hajipange asikate tamaa..!

    Jibu

    Messi na Ronaldo watabaki kua juuuuu

    Jibu

    Nawakubali wote

    Jibu

    Yuko sahihi

    Jibu

    Wanaweza mana tunaona walivyo onyesha uwezo wao msimu huu kama wataweza kuongeza juhudi wataweza kuwapita kabisa

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.