Wamezoea kumuita ‘The King’ wanapokuwa mazoezi. Katika kudhihirisha ufalme wake, Kingsley Coman akawatoa machozi Neymar na Mbappe.
Mchezo wa fainali ya Ligi ya Mabingwa – UEFA kati ya PSG na Bayern Munich uligubikwa na majina ya mastaa wa PSG , Neymar na Mbappe. Ila kama ilivyokawaida, mpira unadunda dakika 90. Haikuwa Lewandowski wala nyota wa PSG ambao wamefanya usiku uwe wa aina yake ila ni Kingsley Coman – The King
Katika badiliko pekee kwenye kikosi cha Hans Flick, Coman alichukua nafasi ya Ivan Perisic kama winga wa kushoto. Goli lake la kichwa lilitosha kupeleka shangwe Ujerumani na kuwaacha Ufaransa wakitoa machozi.

Kingsley Coman shujaa wa Bayern Munich.
“Nina furaha isiyokifani lakini pia ninawahurumia PSG. Inaniuma kidogo japokuwa mimi ni Bayern 100%” amesema Kingsley Coman.
“Pengine msimu huu [Coman] ametoka kwenye vivuli vya Ribery na Robben. Ana kipaji cha hali ya juu na amekionesha leo, anaweza kufunga magoli.” amesema Hans Flick.
“Kwa yeye kufunga lile goli baada ya kuwa majeruhi kwa muda mrefu, ni jambo la faraja kubwa” amesema Serge Gnabry.
“Tulikuwa tunafikiria mabadiliko mawili ambayo pengine Bayern wangeyafanya, lakini tulishangazwa kuona Coman ameanza. Perisic alifanya vizuri kwenye michezo yao iliyopita, kulikuwa na kasi kubwa na kutumia muda mwingi kujilinda.” amesema kocha wa PSG – Thomas Tuchel.

Coman aligusa mpira mara 38 na kumpatia wakati mgumu beki wa kulia wa PSG – Thilo Kehrer. Muda wake wa kufanya maajabu ulionekana kipindi cha pili baada ya kupachika goli na kumfanya kuwa Mfaransa wa 5 kufunga goli kwenye Fainali ya UEFA na wa kwanza kufunga goli dhidi ya timu ya Ufaransa.
Beti Mbio za Mbwa Mubashara
Hii ni rahisi zaidi! Hapa USHINDI unaupata kwa kuchagua mbwa anayeshinda mbio na machaguo mengine yenye odds tamu.


warda
Kwa kweli Coman anastahil kuwa mfalme#Meridianbettz
felister
kwa yeye kufunga lile goli baada ya kuwa majeruhi kwa muda mrefu ni jambo kubwa
rama
Maoni:hongela sana bayern kwa ubingwa mumekuwa na kikosi bora sana msimu huuu
Adelta
Coman Yuko vizuri anastahili kuitwa mfalme@meridianbettz
Mwanahamisi
Coman Yuko vizuri
magdalena
lile goal alilopiga lilikuwa balaa ata psg hawakulitegemea
Tatu
King coman watoa machozi neymar na mbappe tatizo PSG walijiamini sana walikuwa ajui kama mpira unadunda na matokeo dk 90 walichokitaka wamekipata hongera bayern
Lydia Emmanuel Magoti
Kiukweli Coman Anajua yupo vizuri kwenye kaz yake anastairi pongez
Khadija
comani yupo vizuri#meridianbettz
aisha
Comani anajua sana namkubali mnoo
Salma ngende
Anastahili ilo
Furahav
Namkubali sana coman.
Saupha mohamed
Coman yupi vizuri
Issa
Coman alifanya jambo sahihi na kwa wakt sahihi bayern walistahili
Ernest
Kingsley Coman ni hazina kubwa sana kweli ulimwengu wa soka na kama bado ataendelea kuwepo kwenye ubora wake basi tutegemee makubwa kutoka kwake
Gabriel
Hii gemu kiukwel ilikuwa ngumu sana kutabirika maana timu zote zilijipanga kimashindano
Fatuma kasomo
Yupo vizuri
Povel
Congrat Kingsley COMAN man of the man Usiku wa fainal ya ligi ya Mabingwa ulaya
Hope mwaikuka
Gud to him
Amiri Kayera
Huy nd alipelek kilio Kwa psg
Rose kapinga
Coman mahiri xana!!!
Genia Sikaluzwe
Yuko vizuri
Sabrina
Yani roho imeniuma sana PSG kukosa ubingwa wamechana mkeka wangu.
Shafii
Kuna msemo unasema yaliyomo yamo hili lili jionesha kabla ya mechi kwamba Bayern ndio bingwa kwa hali yeyote ile.
Theonestina
Yupo vizur
Latifa juma mohamed
Coman Yuko vizuri anastahili kuitwa mfalme@meridianbettz
David Pere
Hii gemu kiukwel ilikuwa ngumu sana kutabirika maana timu zote zilijipanga kimashindano
farida ahmadi
Hanaweza pia na hanajua coman ni mchezaji mzuri Sana
Rehema
Safi
Dorophina
Coman is talent player
Sauda
Anastahili kuwa mfalme
Zeiyana
PSG wanaweza kumuita Coman ndio mchawi wao..!hawaamini walicho kiona
Caroline
Coman kweli ni.THE KING
Nasra
Anastahili haswaa
Samiah
Yupo vzr
Fatina mfingi
Yupo vizur kijana!!