Huu ukiwa ni msimu mgumu sana katika historia yake ya kuwepo Barcelona, tangia sakata lile la uhamisho la kiangazi, Lionel Messi anasema kuwa ameamua “Kupambania kila kitu” huko Barcelona msimu huu.
Fowadi huyo wa Argentina alifikisha rekodi ya Pele ya mabao 643 kwa klabu moja na ana nafasi ya kuvunja rekodi tena kwa kuandika rekodi ya peke yake wakati Barcelona inakabiliana na Real Valladolid Jumanne, na kumzidi mtangulizi wake Pele.
Messi, ambaye alikuwa karibu na kuondoka Barcelona mnamo Agosti wakati wa sintofahamu baina yake na uongozi wa kilabu, anasema ameongeza tena umakini kwa msimu uliosalia.

“Ukweli ni leo mimi naisikia vizuri, lakini nilikuwa najisikia vibaya wakati wote wa majira ya joto, kabla ya majira ya joto, kwa sababu ya jinsi msimu ulivyomalizika,” alinukuliwa akizungumza na kituo cha Televisheni cha Uhispania La Sexta.
“Ndipo ikaja kile kilichotokea wakati wa kiangazi, burofax na yote hayo kwa pamoja. Halafu kisha nikaanza nayo mwanzoni mwa msimu. Siku hizi, najisikia vizuri.”
Messi amesema bado hajapoteza muelekeo na Barcelona na anaziingatia kile kinachotegemewa kutoka kwake, anajiona bado ana ari ya kufanya vyema licha ya yale yaliyotokea na ukweli kuwa klabu inapitia kipindi kigumu.
VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini???



Mariam mtandama
Habari njema
Issa
Mess anabak jina mpira umeisha
Adelta
Messi Bado yupo vizuri ma anazidi kuwa
Karibu na Barcelona
Caroline
Uyo ndo Messi
Angelina
Goodupdate
Rahmal
Messi Bado Yuko vizuli
Hopemwaikuka
Uamuz mzur messi
Saupha mohamed
Messi yupo vizuri
Tatu
Messi kama messi
Mwanahamisi
Messi yuko vizuri
Lydia Emmanuel Magoti
Nikweli lazima usiwe poa Jembe zote nichangamoto zakwenye soka
warda
Hata mie kama Messi msimu wa joto najisikiaga vibaya sana