Morrison Aifuata Yanga Bukoba

Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Bernard Morrison leo ameanza safari kuelekea Bukoba kuungana na wachezaji wenzake ambao wana mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Kagera Sugar, Julai 8.

Mchezo huo unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kwa kuwa Yanga ilipoteza mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Uhuru, kwa kufungwa mabao 3-0, utapigwa Uwanja wa Kaitaba.


Jana, Julai 5 wakati Yanga ikilazimisha sare ya bila kufungana na Biashara United ilikosa huduma ya Morrison ambaye aliachwa Dar.

Kocha Mkuu wa Yanga, Luc Eymael alisema kuwa iwapo atamhitaji Morrison kwenye mchezo dhidi ya Kagera Sugar atawaambia viongozi wampeleke.

Kupitia ukurasa wake wa Istagram Morrison amewaambia mashabiki wake kuwa habari Bukoba, niambieni kile ambacho sijaskia.

Morrison amefunga jumla ya mabao matatu na kutoa pasi tatu ndani ya Ligi Kuu Bara.

48 Komentara

    Drama za Morison hazileti afya ya soka letu. Kama mchezaji ana mkataba na timu ni lazima aheshimu hilo bila kubembelezana kama hili la Morrison#meridianbettz

    Jibu

    Morrisoni nenda kama angalau unaweza ukaleta mabadiliko kwa yanga maana hali sio nzuri kabisa

    Jibu

    Nenda marrison ukatuletee mabadiliko

    Jibu

    Pamoja na kuwafuata Yanga Bukoba ,Morrison anawachanganya sijui amegundua wanamuhitaji sana, maana yake kama timu zetu anazipima akili ila na timu zenyewe bado hawajielewi .

    Jibu

    Morison n mchezaj mzr sema sasa naona anapagawa na kelele na ushawishi wa timu pinzani ndio tabu ya wachezaji wa kigen wanapenda kusujudiwa wakiona timu kadhaa kubwa na vyombo.vya habar zikimzungumzia yeye ana jiona ndio mfalme inabidi waheshimu mikataba na sheria za club #meridianbet

    Jibu

    Morrison anazingua sana na tatzo viongozi wake wanalea Sana Ayo mambo ndo maama heshima katika timu anakuwa Hana anafanya anavyotaka yeye

    Jibu

    Aende tu akaongeze nguvu Mana kwa yanga Hali si shwari

    Jibu

    Morrison anayumba Bado ajakielewa Nini anakifanya mchezaji anahejielea Hawez kukaa sehemu bila usajili izo no drama anatuchezea huyo

    Jibu

    Jembe limerejea sasa simba kazi mnayo

    Jibu

    Morrison yupo poa ila anahitaji matunzo pale yanga ili asiweze kutoka hapo yanga,jamaa anajua sana na hana mbadala pale yanga ndio maana analinga sana

    Jibu

    Morrison ni jembe, vema akienda huko inawwsekan yanga wakafanya vzr Zaid maan young African Hali c poa wananiboa tu wanapoanza kutangulia kwa magoli halafu wanaishia njian nenda baba okoa jahaz.

    Jibu

    Morrison fundi sana anaipa yanga matokeo inapobidi

    Jibu

    safari njema Morrison

    Jibu

    Morrison fundi sana anaipa yanga matokeo inapobidi ana mchango mkubwa

    Jibu

    Ni vizr coz ndo timu anayo itumikia kwa sasa.

    Jibu

    Ni habari njema kwa wanayanga Morrison ni mchezaji mzuri.

    Jibu

    Afadhali aifuate atafanya jambo la maana sana.

    Jibu

    Habari njema kwa wanayanga#meridianbettz

    Jibu

    Nenda Morrison ukatulee mabadiliko

    Jibu

    Morrison habari zake bado ni zengwe tuu

    Jibu

    Morrisn habari zake sizielewagi

    Jibu

    Morrison anatakiwa kuiheshimu timu sio kuleta drama tu acheze akitaka yeye

    Jibu

    Safari njema

    Jibu

    Morrison habar nyngne wapinzan wajipange

    Jibu

    Saf San mchango wake unaitajik san

    Jibu

    Yani hapo ulw msemo hakuna mchezaji mkubwa zaidi ya timu umeaminiwa na morison mwenyewe kakubali yaishee

    Jibu

    Huyu morrison majanga matupu.

    Jibu

    Ni jambo zuri kwa wana yanga kuongeza nguvu kwenye kikosi kwani tunafahamu kua Morison ni mchezaji mzuri na mzoefu.

    Jibu

    Mjini Kaitaba kutakua hakutoshi iyo july8

    Jibu

    Maoni:Bora akaungane nao labda tutapata matokeo ya kuidhisha

    Jibu

    Nenda ukawasaidie haoo yanga

    Jibu

    Vizuri kwenda kuongeza nguvu

    Jibu

    Habari njema kwa sisi wapenzi wayanga

    Jibu

    Non pro kitendo alichofanya kilikuwa cha ajabu sana

    Jibu

    Aende akafanye vizuri Sasa sio akalete dharau

    Jibu

    Nice

    Jibu

    Morrisn habari zake sizielewagi

    Jibu

    Huyu nae anahangaika#Meridianbettz

    Jibu

    Kwenye mechi iyo najua halitakosekana gori la morison lazima kieleweke

    Jibu

    Morrison ni mchezaji mzuri sana kwa timu ya yanga lakini kwa mchezaji huyu namuona kama anajitenga kutokana na ujuaji wake wa Mpira au vishawishi kutoka kwa timu pizani mana amejiweka nyuma sana kuacha na timu Mara nyingine hivyo sijui kwa sababu gani hili linatokea kwake tu na isiwe wengine kama ingekuwa kwa nchi nyingine angeshapigwa faini au kufungiwa kushiriki katika timu kadhaa.

    Jibu

    Good 👍

    Jibu

    Jamaa anazingua kwer sijui anajikuta nani vile

    Jibu

    Yote heri

    Jibu

    Tunamkarbisha sana 👍 mwana mpotezo asijal YANGA tunamkarbisha vzur na tutamchinjia ng’ombe mnono

    Jibu

    Hao watani zetu hawatutishi

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Nikheri pia

    Jibu

    Jambo jema

    Jibu

Acha ujumbe