Neymar Afungiwa Kucheza Mechi 2

Nyota wa PSG, Neymar amefungiwa kucheza mechi 2 kufuatia kadi nyekundu aliyoipata kwenye mechi waliyopoteza dhidi ya Marseille.

Nyota huyu alikuwa mmoja wa wachezaji watano waliolimwa kadi nyekundu kwenye mechi ambayo PSG walichapwa bao 0-1.

Neymar alipewa kadi nyekundu baada ya kuthibitishwa na VAR kuwa alimpiga nyuma ya kichwa mpinzani wake Alvaro Gonzalez, suala ambalo katika kulipana visasi dimbani, baadaye likaleta taharuki na mabishano makubwa dakika za lala salama za mchezo.

Baada ya mechi nyota huyu alilalamika kuwa Gonzalez alimtupia matamshi ya kibaguzi, na yeye alishindwa kuvumilia hilo. Klabu ilitoa tamko la kuwa wanasimama pamoja na Neymar kama alitamkiwa matamshi ya kibaguzi.

Baada ya kikao cha nidhamu maamuzi ya kufungiwa mechi mbili yana waathiri Neymar na Leandro Paredes, wakati Layvin Kurzawa akifungiwa kucheza mechi 6. Dario Benedetto na Houssem Aouar wamepewa adhabu ya kukosa mechi moja huku Jordan Amavi akizikosa mechi 6.

Angel Di Maria anatarajia kuonekana kwenye kikao cha nidhamu Jumatano ijayo, wakati Alvaro Gonzalez akiwa chini ya chunguzi na LFP.


 

SHINDA NA MERIDIANBET!

Tengeneza pesa kidijitali kwa kubashiri mbio za farasi hapa Meridianbet! Chagua nani ashinde, unakusanya mkwanja.

Cheza Sasa.

 

38 Komentara

    Duuuh hatari sana jamani wachezaji wete waliofungiwa katika timu zao wrote wanategemewa katika kikosi huu ubaguzi utaisha lini mungu ibariki Tanzania yetu yenye amani

    Jibu

    Hayo Ni majanga wachezaji wote wanategemewa na klabu zao sijui itakuwaje

    Jibu

    Sio poa

    Jibu

    Ni kweli kama Professional player Neymar hakutakiwa kureact namna ambavyo alifanya na wachezaji wengine pia lakini kama Neymar alitamkiwa maneno ya Kibaguzi hili swala linatakiwa liangaliwe kwa undani zaidi na kupatiwa ufumbuzi

    Jibu

    Hapa Kazi ipo @meridianbettz

    Jibu

    sad news

    Jibu

    Duh hatarii

    Jibu

    Hili swala zito

    Jibu

    Pole sana Neymar

    Jibu

    Dah majanga gani haya

    Jibu

    Duuh hatari

    Jibu

    jamani majanga gani tena haya#meridianbettz

    Jibu

    Lakini wasikae upande mmoja.na Yule aliemtamkia maneno ya kibaguzi achukuliwe hatua

    Jibu

    Sheria imefuata mkondo wake,Soka ni mchezo wa furaha sio kulipizana kisasi uwanjani kwa ugomvi.P S G mwaka huu watakua na wakati mgumu sana kutwaa ndoo ya ya Ufaransa

    Jibu

    Duuh atari

    Jibu

    PSG kwa sasa wanaali ngumu hadi kuja kufuzu kombe la ubingwa ufarasa kazi ya ziada ifanyike

    Jibu

    Duu noma Sana wamechekecha mpaka Sheria ufata mkondo PSG wangalie Sana kabumbu wanalo licheza

    Jibu

    Sheria imefuata mkondo wake ,hakutakiwa kumfanyia hivyo ni hatari sana

    Jibu

    Kiukwel Gonzalez alimtupia matamshi ya kibaguzi na yeye alishindwa kuvumilia hilo Klabu ilitoa tamko la kuwa wanasimama pamoja na Neymar kama alitamkiwa matamshi ya kibaguzi hiyo sheria ungeangalia upande wa pili

    Jibu

    Duuuh huu ni mkosi sasa

    Jibu

    Sijui itakuaje mbona majanga

    Jibu

    Mmh mbona kisanga

    Jibu

    Duuuh majanga

    Jibu

    Kaz kaz

    Jibu

    Majanga haya

    Jibu

    Inasikitisha Sana

    Jibu

    Duuuh

    Jibu

    Uzur adhab aijawa kubwa zaid

    Jibu

    Duuuh

    Jibu

    Duuuh hatari sana jamani wachezaji wete waliofungiwa katika timu zao wrote wanategemewa katika kikosi huu ubaguzi utaisha lini mungu ibariki Tanzania yetu yenye amani

    Jibu

    Majanga

    Jibu

    Unakumbushwa tuu ujue wajibu wako,na ujifunze kutokana na makosa uliyoyafanya!!

    Jibu

    wamefanya vyema sana juu ya kufanya maamuzi ayo itakuwa funzo kwa watu wengine

    Jibu

    Hasira hasara kaikosti timu tayari licha ya kukosewa na mchezaji wa timu pidhani

    Jibu

    Eeh ! Sio poa

    Jibu

    Sio maamuz sahih kwa neymar ubaguz umefanyika kwake

    Jibu

    Siyo Sawa kabisa vipi ili tatizo la ubaguzi kwa namna hii litaisha kwer

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.