Baada ya kichapo cha aibu cha 4-1 dhidi ya Watford, shinikizo la meneja Ole Gunnar Solsjaer kuondoka klabuni hapo limeongezeka mara dufu. Wakati huu hata viongozi wa juu wa United kushindwa kuvumilia.
Taarifa zinasema kwisha habari yake, maamuzi rasmi bado hayajawa bayana lakini bodi ya klabu imefanya maamuzi ya kumtimua, maamuzi yanayotajwa kupitishwa na wamiliki wa klabu.
Ole Gunnar ni mmoja wa makocha wenye bahati, kwa kuzingatia uhusiano wa Man United na makocha wao inapofikia hali kama ya sasa.

Baada ya mechi, kikao cha dharura cha Bodi ya Manchester United kiliitwa kwa ajili ya kumjadili Ole Gunnar, ambaaye ni majuzi tu amesaini mkataba mpya wa miaka mitatu.
Katika ajenda zilizowekwa, ilikuwa ni kujadili malipo ambayo klabu italazimika kulipa kwa ajili ya kusitisha mkataba, na mambo ya ziada ya kuinusuru klabu.
Kwa mujibu wa mwandishi wa michezo, Fabrizio Romano, bodi ya klabu tayari imeshafanya maamuzi ambayo yamepitishwa na wamiliki wa Manchester United – The Glazer Family na ni masuala ya kiutaratibu tu ambayo yanasubiliwa.
Unasababu milioni za kucheza unavyotaka ukiwa na mabingwa meridianbet, lakini unasababu moja ya kushinda mamilioni katika kasino za mtandaoni za meridianbet. Mchezo maridhawa wa Crazy Time unakupa sababu hizo kuwa mmoja wa washindi leo hii.


