Bosi wa muda wa Manchester United,Ralf Rangnick anasema sintofahamu inayosababishwa na Covid-19 imeathiri maendeleo yake tangia alipochukua majukumu ya umeneja klabuni hapo.
Rangnick hajafungwa kwenye mechi nne tangia alipomrithi Ole Gunnar Solskjaer mwishoni mwa mwezi Novemba.
Kwa mujibu wa bosi huyu, mlipuko wa Covid-19 ambao umepelekea kufungwa kwa kituo cha mazoezi cha Manchester United Carrington, pamoja na kusogezwa mbele kwa mechi mbili kumefanya kazi yake kuwa ngumu zaidi.

Rangnick anaamini kuwa bado ameshindwa kufikia malengo yake, sababu kubwa ikiwa ni Covid;
“Kila kocha. kila kocha mwenye nia ya mafanikio makubwa, na hakuna utofauti kati yangu na makocha wengine kwenye eneo hilo, wanataka kupiga hatua za haraka na hatua kubwa kusonga mbele. Lakini ili uweze kufanya hivyo, unapaswa kuwa na uwezo wa kufundisha”
Unaanzaje siku yako katika msimu huu wa sikukuu, mchongo upo meridianbet kasino. Sloti pendwa ya Sahara Richies inaweza kukufanya ukawa milionea katika kufunga mwaka huu, Jiunge na ufurahie kasino maridhawa kutoka nyumba ya mabingwa.

CHEZA HAPA

