Shirikisho la soka la Belgium (KBVB) limetangaza kuwa Roberto Martinez amesaini mkataba kusalia Belgium kama kocha mkuu hadi 2022.
Martinez aliteuliwa na Belgium mwaka 2016, mkataba wake mpya unampa nafasi ya kuendelea kusalia klabuni hapo hadi mwaka wa Kombe la Dunia la Quatar 2022.
Kocha huyu Mhispania aliwaongoza kikosi cha Belgium maarufu kama “Golden Generation”, huku uswahilini tunaweza kusema “Kizazi cha Dhahabu” hadi kufikia nusu fainali za Kombe la Dunia Urusi mwaka 2018 ambako Ufaransa waliamua kuwabania riziki kwa kuwapa kichapo kabla ya kuwalaza Uingereza na kuchukua ubingwa wa dunia.

Mkataba wake wa sasa ulikuwa unaisha baada ya michuani ya Euro 2020 ambayo imesogezwa mbele kwa mwaka mmoja zaidi kwa sababu ya janga la corona.
Belgium ambao kwa sasa wapo kwenye kilele cha FIFA kwa timu bora zaidi, walikuwa moja ya timu zilizotarajiwa kuondoka na ubingwa wa dunia baada ya kufanya vyema katika hatua za awali toka kufuzu mpaka walipoingia nusu fainali.
Tangazo la Belgium limenogeshwa na Hazard!
Tangazo limeambatana na video fupi ya kapten wa Belgium na nyota wa Real Madrid, Eden Hazard akicheza gemu ya video maarufu ya FIFA huku akivunga kama anapokea simu ya nchezaji mwenzake Romelu Lukaku.
Kwenye video fupi Hazard anasema:
“Kocha amesaini! Kocha amesaini, ole ole ole. Mambo Romelu, umeona kocha kasaini? ndiyoo si ni taarifa njema hizi! Haya kwaheri”
Belgium na Martinez wanatarajia kuongea na vyombo vya habari Jumatano hii ili kuzungumzia suaola la mkataba wake mpya.


Hamidu
Coach Bora Robert Martinez..amestahili kuongezewa mkataba.#meridianbettz
Khadija
ahsante meridian kwa taarifa#meridianbettz
Neema juma
Duuu asante kwa kutujuza #meridianbet
frank patrick
Martinez anafanya vizuri sana kwenye machaguzi yake ya wachezaji na ndio maana Belgium wanafanya vizuri sana
winfrida
inapendeza na ni hatua nzuri
Antony Luseno
Good news to Belgium team #meridianbettz
Carolyne
Hongera yake
Povel
Hongera Martinez @robArt (kibala) kwa kuongezwa mkataba kila la kheri na mafanikio tele kwny majukumu yako ya kazi thanks meridian kwa habar za michezo na burudani
Shafii
Safi sana Martinez ni bonge la kocha anastahili kuendelea kuinoa Belgium
Zeiyana iddi
Coach mzuri sana..!nategema mabadiliko kutoka kwako
David pere
Ni kocha nzuri Sana akiwa kwenye kazi yake
Ester
Inapendeza sana kwa hatua aliyo ifikia ya kuwa kocha mkuu
Tahiya
Good news
Mwajuma
Ni kocha anaejituma sana anastahili kuongezwa mkataba
Ernest
Anastahili pongezi kwa kazi nzuri.
aisha
Ni kocha mzuri sana ambaye anajua kujituma safi sana
Mwanaidi
Habari nzr asanteni kwa kutujulisha
Swai
Anastahili
Genia skaluzwe
Mambo mazuri hayo
sylvester
He deserve it #meridianbettz
Kenani
Inapendeza sana
SADICK
Ni Kocha mzuri na amepata mafanikio kiasi fulani lakini anahitajika kufanya zaidi ili kizazi cha dhahabu kilete vikombe #Meridianbettz
Rehema Dickson
Yuko vizuri hana masihala kwenye kazi yake,,namkubali kinoma💪
Aziza mushi
Yupo vizuri.
Asia Abdy
Good news
Samira
Ahsanteni kwa kutuhabarisha meridianbet
Gabriel
Habar njema # meridianbet
Emmy cleopa
Hongera zake
Christopher
AMeisaidia timu kwa kiasi kikubwa, vizuri aendelee kuitumikia Belgium kwa awamu nyingine tena
Magdalena
Habari njema kabisa kwa sisi tunaomuelewa Martinez.
#meridianbet
Hidaya Mohammed
Ni habari nzuri sana kwa wapenzi wa soka wa nchini kwao
Adelta
Asante kwa taarifa meridianbet
Theonestina
Hongera yake
Neema juma
Hongera kwakeee kwa kujituma vyema
Elika
Safi sana kocha kwa kuongeza mkataba mwingine
Furahav
Hongera kicha bora.
Salma
Ni habari nzuri
Mariam mtandama
Safi
Lombo
gud newz asante
Theckla
Namkubali Sana Mana ni kocha anayejitambua na asiyekurupuka katika kufanya chaguzi za wachezaji
felister
anastahili pongezi kwake
Mwanahamisi
Hongera yake
Lydia Emmanuel Magoti
Nikocha mzuri Sana hana stairi pongezi
Samiah
Hongera yake
Agness
Asante meridiani kwa taarifa njema