Real na Liverpool Uso kwa Uso kwa Ruiz

Klabu ya Real Madrid inamtaka nyota anayefukuziwa na Liverpool Fabian Ruiz.

Ripoti zimetaja kuwa Real Madrid ni moja ya klabu ambazo zipo tayari kuingia kwenye mbio za kumfukuzia nyota wa Napoli Fabian Ruiz ambaye pia anatajwa kutupiwa kijicho na Liverpool.

Nyota huyu Muhispania mwenye umri wa miaka 24 ambaye aliondoka Real Betis na kutimba Italia alipoungana na Napoli, amekuwa akifanya vizuri sana na kuvutia klabu zingine.

Liverpool tayari walikuwa kwenye windo kumnasa lakini sasa wanakutana na ushindani kutoka kwa Real Madrid wakitarajia pia kumpata ili awasaidie katika safari ya matumaini kule LaLiga.

Klabu zingine zinazovutiwa na staa huyu ni pamoja na klabu ya Man United na Bayern Munich . Kwa mujibu wa wakala wa Ruiz, bwana Alvaro Torres amethibitisha kuwa ameshawasilisha kwa Napoli kuwa klabu ya Real Madrid inataka kumsajili mteja wake.

3 Komentara

    Fabian luiz hana maamuzi yake kwenda Liverpool hama Real Madrid mana zote ni klabu kubwa tyuu na nzuri pia

    Jibu

    Gud news

    Jibu

    Itapendeza

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.